Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Habakuki 1
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Habakuki—Yaliyomo

      • Nabii alilia msaada (1-4)

        • ‘Ee Yehova, mpaka lini?’ (2)

        • “Kwa nini unavumilia ukandamizaji?” (3)

      • Wakaldayo, watumiwa na Mungu kutekeleza hukumu (5-11)

      • Nabii amsihi Yehova (12-17)

        • ‘Mungu wangu, wewe hufi’ (12)

        • ‘Wewe ni safi sana usiweze kutazama uovu’ (13)

Habakuki 1:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Huenda jina hili linamaanisha “Kumbatio Changamfu.”

Habakuki 1:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “huniokoi.”

Marejeo

  • +Zb 13:1
  • +Zb 22:1; 74:10; Ufu 6:10

Habakuki 1:4

Marejeo

  • +Ayu 12:6; Zb 12:8; Mhu 8:11; Isa 1:21; Mdo 7:52, 53

Habakuki 1:5

Marejeo

  • +Isa 28:21; 29:14; Omb 4:11, 12; Mdo 13:40, 41

Habakuki 1:6

Marejeo

  • +Yer 22:7; 46:2
  • +Kum 28:49-51; Yer 5:15-17; 6:22, 23; Eze 23:22, 23

Habakuki 1:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “haki.”

  • *

    Au “heshima.”

Marejeo

  • +Yer 39:5-7; Da 5:18, 19

Habakuki 1:8

Marejeo

  • +Yer 5:6
  • +Yer 4:13; Omb 4:19; Eze 17:3

Habakuki 1:9

Marejeo

  • +Yer 25:9
  • +Isa 27:8; Eze 17:10

Habakuki 1:10

Marejeo

  • +2Fa 24:12
  • +Yer 32:24; 52:7

Habakuki 1:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “nguvu zao ni mungu wao.”

Marejeo

  • +Isa 47:5, 6; Yer 51:24; Zek 1:15
  • +Da 5:1, 4

Habakuki 1:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “sisi hatutakufa.”

  • *

    Au “wakaripie.”

Marejeo

  • +Zb 90:2; 93:2; Ufu 1:8
  • +1Ti 1:17; Ufu 15:3
  • +Kum 32:4
  • +Yer 30:11

Habakuki 1:13

Marejeo

  • +Zb 5:4, 5
  • +Yer 12:1
  • +Zb 35:21, 22

Habakuki 1:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, jeshi la Wakaldayo.

Marejeo

  • +Yer 50:11

Habakuki 1:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kufukiza moshi wa dhabihu.”

  • *

    Tnn., “Kwa maana kupitia hizo fungu lake limetiwa mafuta mengi.”

Habakuki 1:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “kuchomoa upanga wake.”

Marejeo

  • +2Nya 36:17; Nah 3:7

Jumla

Hab. 1:2Zb 13:1
Hab. 1:2Zb 22:1; 74:10; Ufu 6:10
Hab. 1:4Ayu 12:6; Zb 12:8; Mhu 8:11; Isa 1:21; Mdo 7:52, 53
Hab. 1:5Isa 28:21; 29:14; Omb 4:11, 12; Mdo 13:40, 41
Hab. 1:6Yer 22:7; 46:2
Hab. 1:6Kum 28:49-51; Yer 5:15-17; 6:22, 23; Eze 23:22, 23
Hab. 1:7Yer 39:5-7; Da 5:18, 19
Hab. 1:8Yer 5:6
Hab. 1:8Yer 4:13; Omb 4:19; Eze 17:3
Hab. 1:9Isa 27:8; Eze 17:10
Hab. 1:9Yer 25:9
Hab. 1:102Fa 24:12
Hab. 1:10Yer 32:24; 52:7
Hab. 1:11Isa 47:5, 6; Yer 51:24; Zek 1:15
Hab. 1:11Da 5:1, 4
Hab. 1:12Zb 90:2; 93:2; Ufu 1:8
Hab. 1:121Ti 1:17; Ufu 15:3
Hab. 1:12Kum 32:4
Hab. 1:12Yer 30:11
Hab. 1:13Zb 5:4, 5
Hab. 1:13Yer 12:1
Hab. 1:13Zb 35:21, 22
Hab. 1:15Yer 50:11
Hab. 1:172Nya 36:17; Nah 3:7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Habakuki 1:1-17

Habakuki

1 Tangazo ambalo nabii Habakuki* alipokea katika maono:

 2 Ee Yehova, nililie msaada mpaka lini, lakini wewe hunisikii?+

Nitaomba msaada kwa sababu ya ukatili mpaka lini, lakini huingilii kati?*+

 3 Kwa nini unanifanya nione mambo mabaya?

Na kwa nini unavumilia ukandamizaji?

Kwa nini uharibifu na ukatili uko mbele yangu?

Na kwa nini ugomvi na mizozo inaongezeka?

 4 Kwa hiyo sheria haifanyi kazi,

Na haki haitekelezwi kamwe.

Kwa maana mwovu amemzingira mwadilifu;

Ndiyo sababu haki imepotoshwa.+

 5 “Tazameni miongoni mwa mataifa, kazeni uangalifu!

Tazameni kwa mshangao na kustaajabu;

Kwa maana jambo fulani litatukia katika siku zenu

Ambalo hamtaamini hata mkiambiwa.+

 6 Kwa maana tazama, ninawainua Wakaldayo,+

Taifa katili na linalotenda haraka-haraka,

Wanasambaa upesi katika maeneo makubwa sana ya dunia

Ili wachukue kwa nguvu makao ambayo si yao.+

 7 Wanatisha na kuogopesha.

Wanaweka sheria* yao wenyewe na mamlaka* yao wenyewe.+

 8 Farasi wao wanakimbia kasi kuliko chui,

Nao ni wakali kuliko mbwamwitu wakati wa usiku.+

Farasi wao wa vita hukimbia mbele kwa kasi;

Farasi wao hutoka mbali sana.

Wanashuka chini kwa kasi kama tai anayekimbilia chakula.+

 9 Wote huja wakikusudia kutenda ukatili.+

Nyuso zao kwa pamoja ni kama upepo wa mashariki,+

Nao huchota mateka kama mchanga.

10 Wanawadhihaki wafalme

Na kuwacheka maofisa wakuu.+

Wanaicheka kila ngome;+

Wanatengeneza daraja kwa rundo la udongo na kuiteka.

11 Kisha wanasonga mbele kama upepo na kupita humo,

Lakini watakuwa na hatia,+

Kwa sababu wanasema nguvu zao zinatoka kwa mungu wao.”*+

12 Je, wewe si wa tangu milele, Ee Yehova?+

Ee Mungu wangu, Mtakatifu wangu, wewe hufi.*+

Ee Yehova, uliwachagua ili watekeleze hukumu;

Mwamba wangu,+ uliwaweka ili watekeleze adhabu.*+

13 Macho yako ni safi sana yasiweze kutazama uovu,

Nawe huwezi kuvumilia uovu.+

Basi, kwa nini unawavumilia wenye hila+

Na kunyamaza mtu mwovu anapommeza mtu mwadilifu kuliko yeye?+

14 Kwa nini unamfanya mwanadamu awe kama samaki wa baharini,

Kama viumbe wanaotambaa ambao hawana mtawala?

15 Hao wote yeye* huwavua kwa ndoano.

Huwakamata kwa wavu wake wa kukokotwa,

Naye huwakusanya katika wavu wake wa kuvulia samaki.

Ndiyo sababu anashangilia sana.+

16 Ndiyo sababu anatoa dhabihu kwa ajili ya wavu wake wa kukokotwa

Na kutoa dhabihu* kwa ajili ya wavu wake wa kuvulia samaki;

Kwa maana nyavu hizo zimemletea utajiri,*

Na chakula chake ni bora.

17 Je, ataendelea kutoa samaki katika wavu wake wa kukokotwa?*

Je, ataendelea kuyaangamiza mataifa bila huruma?+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki