Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 26:47-50
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 47 Alipokuwa bado akizungumza, tazama! Yuda, mmoja wa wale 12, akaja pamoja na umati mkubwa wakiwa na mapanga na marungu, walikuwa wametumwa na wakuu wa makuhani na wazee wa watu.+

      48 Basi msaliti wake alikuwa amewapa ishara, akisema: “Yule nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni.” 49 Akaenda moja kwa moja kwa Yesu akasema: “Salamu, Rabi!” kisha akambusu kwa wororo. 50 Lakini Yesu akamuuliza: “Mwenzangu, umekuja kufanya nini?”+ Ndipo wakaja na kumkamata Yesu na kumtia nguvuni.

  • Marko 14:43-46
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 Na mara moja, alipokuwa bado akizungumza, Yuda, mmoja wa wale 12, akafika pamoja na umati wenye mapanga na marungu, walikuwa wametumwa na wakuu wa makuhani, waandishi, na wazee.+ 44 Basi msaliti wake alikuwa amewapa ishara waliyokubaliana akisema: “Yule nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni na kuondoka naye akiwa chini ya ulinzi.” 45 Akaja moja kwa moja akamkaribia na kusema, “Rabi!” kisha akambusu kwa wororo. 46 Basi wakamkamata na kumtia nguvuni.

  • Yohana 18:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Sasa Yuda msaliti wake alijua mahali hapo, kwa sababu mara nyingi Yesu alikutana hapo na wanafunzi wake. 3 Basi Yuda akaja na kikosi cha wanajeshi, maofisa wa wakuu wa makuhani na wa Mafarisayo, wakafika hapo wakiwa na mienge, taa, na silaha.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki