Maelezo ya Chini
b Bila shaka, hilo halimaanishi kwamba si sawa kwa Mkristo kwenda kupimwa kujua afya ya mtoto mchanga asiyezaliwa. Kunaweza kuwa na sababu kadhaa za kitiba zinazokubalika Kimaandiko zinazofanya tabibu apendekeze apimwe. Hata hivyo, kupimwa kwingine kwaweza kuhatarisha mtoto, na basi ni jambo la hekima kuongea na daktari kuhusu mambo hayo. Kwa sababu ya kupimwa huko, mtoto akipatikana ana kasoro mbaya sana, wazazi Wakristo katika nchi fulani waweza kukazwa watoe mimba hiyo. Lingekuwa jambo la hekima kujitayarisha kushikilia kanuni za Biblia.