Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Furahia Kujifunza Kibinafsi Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Desemba 1
    • hata ukatega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu; . . .” (Mithali 2:1, 2)

  • Furahia Kujifunza Kibinafsi Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Desemba 1
    • 7. Inapowezekana, kwa nini tunapaswa kuhudhuria na kusikiliza mikutano ya Kikristo?

      7 Je, kweli ‘tunatega sikio’ na kusikiliza kwa makini wakati Neno la Mungu linapofafanuliwa katika mikutano yetu ya Kikristo? (Waefeso 4:20, 21) Je, ‘tunauelekeza moyo wetu’ ili tupate ufahamu? Labda msemaji hana uzoefu mwingi, lakini tunapaswa kumsikiliza kwa makini anapozungumzia Neno la Mungu. Bila shaka, ili kusikiliza hekima ya Yehova, lazima tuhudhurie mikutano ya Kikristo wakati wote inapowezekana. (Mithali 18:1) Hebu wazia jinsi mtu yeyote aliyekosa ule mkutano uliofanywa katika chumba cha juu huko Yerusalemu, Pentekoste 33 W.K. alivyovunjika moyo! Ingawa mikutano yetu si ya pekee kama mkutano huo, Biblia, ambayo ni kitabu chetu kikuu cha mafundisho, huzungumziwa. Kwa hiyo, tunaweza kunufaishwa kiroho na kila mkutano ikiwa tutasikiliza na kufungua maandiko yanayosomwa katika Biblia zetu.—Matendo 2:1-4; Waebrania 10:24, 25.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki