Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Huwafedhehesha Wenye Kiburi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Watu nao watatafuta kimbilio katika majabali na tundu za miamba iliyopasuka katika siku ya hukumu ya Yehova. Kwa hiyo, hatima ya sanamu na wenye kuziabudu itakuwa sawasawa. Kupatana kabisa na unabii wa Isaya, sanamu zisizo na uhai hazikuwaokoa waabudu wake wala Yerusalemu kutoka mikononi mwa Nebukadreza mwaka wa 607 K.W.K.

      14. Katika siku ya hukumu ya Yehova inayokuja juu ya milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli, watu walio na mtazamo wa kilimwengu watafanyaje?

      14 Watu watafanya nini katika siku ya hukumu ya Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo na juu ya sehemu nyingine za milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli? Yamkini wengi wao, wakikabiliwa na hali zinazozorota ulimwenguni kote, watang’amua kwamba sanamu zao hazifai chochote. Badala ya hizo, huenda wakatafuta kimbilio na ulinzi katika mashirika ya kidunia yasiyo ya kiroho, labda kutia ndani Umoja wa Mataifa, yule “hayawani-mwitu wa rangi-nyekundu-nyangavu” wa Ufunuo sura ya 17. “Pembe kumi” za hayawani-mwitu huyo wa ufananisho ndizo zitakazomharibu Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli, ambayo Jumuiya ya Wakristo ndiyo sehemu mashuhuri.—Ufunuo 17:3, 8-12, 16, 17.

  • Yehova Huwafedhehesha Wenye Kiburi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • ili aingie ndani ya pango za majabali, na ndani ya tundu za miamba iliyopasuka, mbele za utisho wa BWANA na utukufu wa enzi yake, atakapoondoka ili aitetemeshe mno dunia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki