Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • “Nimetia Roho Yangu Juu Yake”

      3. Yehova anamtumia Isaya kutoa unabii gani juu ya “mtumishi wangu”?

      3 Yehova anamtumia Isaya kutoa unabii wa kuja kwa mtumishi atakayemchagua mwenyewe: “Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu [“haki,” “NW”].

  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 42:1

  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 4. “Mteule” aliyetabiriwa ni nani, na tunajuaje hivyo?

      4 Mtumishi anayetajwa hapa ni nani? Hatuachwi na shaka. Tunaupata mtajo wa maneno hayo katika Gospeli ya Mathayo, nao umetumiwa kumhusu Yesu Kristo. (Mathayo 12:15-21) Yesu ndiye Mtumishi mpendwa, “mteule.” Yehova aliweka roho yake juu ya Yesu lini? Mwaka wa 29 W.K., wakati wa ubatizo wa Yesu. Maandishi yaliyopuliziwa hueleza kuhusu ubatizo huo, ya kwamba Yesu akiisha kutoka katika maji, “mbingu ilifunguliwa na roho takatifu katika umbo la kiwiliwili kama njiwa ikateremka juu yake, na sauti ikaja kutoka mbinguni: ‘Wewe ni Mwana wangu, mpendwa; nimekukubali wewe.’” Yehova mwenyewe alimtambulisha hivyo Mtumishi wake mpendwa. Huduma ya Yesu iliyofuata na miujiza aliyoifanya, zilithibitisha kwamba kweli roho ya Yehova ilikuwa juu yake.—Luka 3:21, 22; 4:14-21; Mathayo 3:16, 17.

      ‘Atawatolea Mataifa Haki’

      5. Kwa nini maana ya haki ya kweli ilihitajika kueleweshwa wazi katika karne ya kwanza W.K.?

      5 Mteule wa Yehova ‘angetoa,’ au angetokeza wazi haki ya kweli. “Lililo haki atafanya kuwa wazi kwa mataifa.” (Mathayo 12:18) Hakika hilo lilihitajika sana karne ya kwanza W.K.! Viongozi wa kidini Wayahudi walifunza maoni kombo juu ya haki na uadilifu. Walitafuta kupata uadilifu kwa kufuata sheria ngumu-ngumu—nyingi zikiwa zao wenyewe. Haki yao ya kufuatilia sana sheria ilikosa rehema na huruma.

      6. Yesu alijulisha haki ya kweli kwa njia zipi?

      6 Lakini, Yesu alifunua maoni ya Mungu kuhusu haki. Yesu alionyesha kwa mafundisho na maisha yake kwamba haki ya kweli ina huruma na rehema. Ebu fikiria Mahubiri yake yenye sifa ya Mlimani. (Mathayo, sura ya 5-7) Hayo ni maelezo stadi kama nini kuhusu jinsi ya kufuata haki na uadilifu! Tusomapo masimulizi ya Gospeli, je, hatuguswi moyo na huruma ya Yesu kwa maskini na wanaoonewa? (Mathayo 20:34; Marko 1:41; 6:34; Luka 7:13) Alipeleka ujumbe wake wa faraja kwa wengi waliokuwa kama mianzi iliyopondeka, iliyoinama na kupigwa huku na huku. Walikuwa kama utambi unaotoa moshi ukitaka kuzimika, uhai wao ukikaribia kufifia kabisa. Yesu hakuvunja “mwanzi uliopondeka” wala hakuzima “utambi utokao moshi.” Bali, maneno na matendo yake ya upendo na huruma yaliinua mioyo ya wapole.—Mathayo 11:28-30.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki