Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Yehova anasema hivi: “Mimi, BWANA, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa;

  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 42:6,

  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 14. (a) Inaposemwa kwamba Yehova anashika mkono wa Mtumishi wake aliyekubaliwa, hiyo ina maana gani? (b) Huyo Mtumishi Mteule ana kazi gani?

      14 Muumba Mtukufu wa ulimwengu mzima, Mpaji na Mwendelezaji wa uhai, anashika mkono wa Mtumishi wake Mteule na kuahidi kumsaidia kabisa wakati wote. Ni uhakikishio mzuri, wee! Tena, Yehova anamlinda salama ili amtoe awe “agano la watu.” Agano ni mkataba, mapatano, ahadi nzito. Ni amri hakika. Ndiyo, Yehova amemfanya Mtumishi wake “rehani kwa hao watu.”—An American Translation.

      15, 16. Yesu alitumikiaje akiwa “nuru ya mataifa”?

      15 Akiwa “nuru ya mataifa,” Mtumishi aliyeahidiwa ‘atafunua macho ya vipofu’ na kuwakomboa “wale walioketi gizani.” Ndivyo Yesu alivyofanya. Yesu alitukuza jina la Baba yake wa kimbingu kwa kuishuhudia kweli. (Yohana 17:4, 6) Alifunua wazi uwongo mwingi wa kidini, akahubiri habari njema za Ufalme, akawafungulia mlango wa uhuru wa kiroho wale waliokuwa katika utumwa wa kidini. (Mathayo 15:3-9; Luka 4:43; Yohana 18:37) Alitoa onyo la kutofanya kazi za giza na kumfichua Shetani kuwa “baba ya uwongo” na “mtawala wa ulimwengu huu.”—Yohana 3:19-21; 8:44; 16:11.

      16 Yesu alisema hivi: “Mimi ni nuru ya ulimwengu.” (Yohana 8:12) Alipata kuwa nuru hiyo kwa njia ya wazi sana alipotoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kuwa fidia. Hivyo aliwafungulia njia wale wenye kudhihirisha imani ili wapate msamaha wa dhambi, uhusiano unaokubalika pamoja na Mungu, na tazamio la uhai wa milele. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Kwa kuendeleza ujitoaji mkamilifu wa kimungu maisha yake yote, Yesu aliiunga mkono enzi kuu ya Yehova, akathibitisha Ibilisi ni mwongo. Kweli Yesu alikuwa mfunguaji wa macho ya vipofu, na mkombozi wa wale waliotiwa katika gereza la giza la kiroho.

      17. Sisi tunatumikia tukiwa wachukua-nuru kwa njia zipi?

      17 Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Nyinyi ndio nuru ya ulimwengu.” (Mathayo 5:14) Je, sisi pia si wachukua-nuru? Kwa njia yetu ya maisha na kazi yetu ya kuhubiri, tuna pendeleo la kuelekeza wengine kwa Yehova, Chanzo cha nuru ya kweli. Kwa kumwiga Yesu, tunajulisha jina la Yehova, tunaiunga mkono enzi Yake kuu, na kutangaza kwamba Ufalme Wake ndio tumaini pekee kwa wanadamu. Pia, sisi tulio wachukua-nuru tunafunua uwongo mwingi wa kidini, tunatoa onyo juu ya kazi chafu za giza, na kumfichua Shetani, yule mwovu.—Matendo 1:8; 1 Yohana 5:19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki