-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Maana hujiita wenyeji wa mji mtakatifu, hujitegemeza juu ya Mungu wa Israeli; BWANA wa majeshi ni jina lake.” (Isaya 48:1, 2) Unafiki kama nini!
-
-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Kabla ya kuhamishiwa Babiloni, Wayahudi walimwabudu Yehova kwenye “mji mtakatifu,” Yerusalemu. Lakini ibada yao haikuwa ya moyo mweupe. Mioyo yao ilikuwa mbali sana na Mungu, na vitendo vyao vya ibada vilikuwa ‘si vya kweli, wala si vya haki.’ Hawakuwa na imani kama ile ya wazee wa ukoo.—Malaki 3:7.
4. Ni ibada ya aina gani inayompendeza Yehova?
4 Maneno ya Yehova yanatukumbusha kwamba ibada haipaswi kuwa desturi ya kijuujuu tu. Ni lazima ifanywe kwa hisia za moyoni. Utumishi wa kuonyesha tu—labda unaofanywa ili kuwafurahisha au kuwavutia wengine tu—si “vitendo vya ujitoaji-kimungu.” (2 Petro 3:11) Ibada ya mtu haikubaliki kwa Mungu eti kwa sababu tu mtu anajiita Mkristo. (2 Timotheo 3:5) Ni muhimu kutambua kwamba Yehova yuko, lakini huo ni mwanzo tu. Yehova anataka ibada ya nafsi yote, inayoongozwa na upendo wa kina kirefu na uthamini.—Wakolosai 3:23.
-