-
“Wakati wa Nia Njema”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hata watu mashuhuri na wenye uweza mwingi kutoka mataifa mengine, kama vile “wafalme” na “mabinti-wafalme,” wanawasaidia Waisraeli katika safari yao ya kurudi huko. (Isaya 49:23a, “NW”) Wafalme Waajemi, Koreshi na Artashasta Longimano, pamoja na watu wa nyumba zao wanakuwa miongoni mwa wasaidizi hao. (Ezra 5:13; 7:11-26) Halafu maneno ya Isaya yanatumika kwa njia nyingine tena.
-
-
“Wakati wa Nia Njema”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Katika wakati ufaao, kabila zote za dunia—hata jamii za watawala wa leo—zitalazimika kuuinamia utawala wa Mesiya. (Zaburi 2:10, 11; Danieli 2:44) Matokeo yatakuwa nini? Yehova anasema hivi: “Nawe utajua ya kuwa mimi ni BWANA, tena waningojeao hawatatahayarika.”—Isaya 49:23b.
-