-
“Wakati wa Nia Njema”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Ndiyo. Yehova anawahakikishia hivi: “Hata jeshi la wafungwa wake aliye hodari watapokonywa mikononi mwake, na mateka yake aliye jabari wataokoka.” (Isaya 49:25a) Uhakikisho huo unafariji kama nini! Zaidi ya hilo, Yehova huwaonyesha watu wake nia njema kwa kujiwajibisha sana kuwalinda. Yeye anasema waziwazi hivi: “Nitateta na yeye atetaye nawe, nami nitawaletea wana wako wokovu.” (Isaya 49:25b) Wajibu huo ungali upo. Kama ilivyoandikwa kwenye Zekaria 2:8, Yehova anawaambia watu wake hivi: ‘Yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho langu.’ Ni kweli kwamba sasa tunafurahia kipindi cha nia njema, wakati ambao makundi-makundi ya watu kotekote duniani yana fursa ya kumiminika yakienda kwenye Sayuni wa kiroho. Hata hivyo, kipindi hicho cha nia njema kitafikia mwisho.
-
-
“Wakati wa Nia Njema”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
30. Yehova amewafanyia watu wake maokozi gani, na bado atafanya nini?
30 Maneno hayo yalitumika kwanza Yehova alipomtumia Koreshi kuwaweka watu Wake huru kutoka katika utumwa wa Babiloni. Yalitumika jinsi hiyo hiyo mwaka wa 1919 Yehova alipomtumia Mwana wake mtawazwa, Yesu Kristo, kuwafungua watu Wake kutoka utumwa wa kiroho. Hivyo, Biblia huwataja wote wawili, Yehova na Yesu, kuwa waokozi. (Tito 2:11-13; 3:4-6) Yehova ni Mwokozi wetu, na Yesu, aliye Mesiya, ni ‘Wakili wake Mkuu.’ (Matendo 5:31) Kweli Mungu amefanya maokozi mazuri ajabu kupitia Yesu Kristo. Yehova huzitumia habari njema kuwaweka huru watu walio na mioyo ya kupenda haki kutoka katika utumwa wa dini ya uwongo. Yeye huwakomboa kutoka katika utumwa wa dhambi na kifo kupitia ile dhabihu ya fidia. Mwaka wa 1919 aliwatoa ndugu za Yesu katika utumwa wa kiroho. Kisha ataokoa umati mkubwa wa wanadamu waaminifu kutoka kwenye uharibifu utakaowapata watenda-dhambi katika vita ya Har-Magedoni inayokaribia kasi.
-