-
Siku ya Hukumu ya Yehova I Karibu!Mnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
-
-
Na huko utajiri wao utakuwa mateka, na nyumba zao zitakuwa ukiwa; naam, watajenga nyumba, lakini hawatakaa ndani yake; nao watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.”—Sefania 1:12, 13.
-
-
Siku ya Hukumu ya Yehova I Karibu!Mnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
-
-
16. Ni nini ambacho kingetukia wakati ambapo hukumu ya Mungu ingetekelezwa dhidi ya Yuda, na kujua hivyo kwapasa kutuathirije?
16 Waasi-imani wa Yuda walionywa kwamba Wababiloni wangepora mali zao, wangefanya nyumba zao ukiwa, na kutwaa matunda ya mashamba yao ya mizabibu. Mali za kimwili hazingekuwa na thamani yoyote wakati ambapo hukumu ya Mungu ingetekelezwa dhidi ya Yuda. Ndivyo itakavyokuwa siku ya hukumu ya Yehova itakapoujia mfumo huu wa mambo. Kwa hiyo, na tuwe na mtazamo wa kiroho na ‘kuweka hazina mbinguni’ kwa kuendelea kutanguliza utumishi wa Yehova maishani mwetu!—Mathayo 6:19-21, 33.
-