-
‘Yule Mtumwa Mwaminifu’ Apita Mtihani wa Ukaguzi!Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 1
-
-
Mfano wa Talanta
12. (a) Yesu alitumia mfano gani kuhusu sifa ya uaminifu? (b) Mtu ‘aliyeenda ng’ambo’ ni nani?
12 Baada ya kutoa mfano kuhusu busara, Yesu alitoa mfano mwingine kuhusu sifa ya uaminifu. Alisema: “Ni kama wakati ambapo mtu, akiwa karibu kusafiri ng’ambo, aliwaita watumwa wake na kuwapa mali zake.
-
-
‘Yule Mtumwa Mwaminifu’ Apita Mtihani wa Ukaguzi!Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 1
-
-
Mtu anayetajwa katika mfano huo ni Yesu mwenyewe, ambaye ‘alienda ng’ambo’ alipopanda mbinguni mwaka wa 33 W.K. Lakini kabla ya kupanda mbinguni, Yesu aliwapa wanafunzi wake waaminifu “mali zake.” Jinsi gani?
13. Yesu alitayarishaje shamba kubwa la utendaji na kuwapa ‘watumwa’ wake ruhusa ya kufanya biashara?
13 Wakati wa huduma yake duniani, Yesu alianza kutayarisha shamba kubwa la utendaji kwa kuhubiri habari njema za Ufalme katika nchi yote ya Israeli. (Mathayo 9:35-38) Kabla ya ‘kwenda ng’ambo,’ aliwapa wanafunzi waaminifu shamba hilo akisema: “Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.” (Mathayo 28:18-20)
-