Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi Kamwe
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
    • 1 Wakorintho 13:4-8

  • Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi Kamwe
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
    • Ona kwamba katika mstari wa 8, Paulo alisema kwamba zawadi za roho, kutia ndani kutoa unabii na kusema kwa lugha, zawadi ambazo zilitumiwa mwanzoni mwa kutaniko la Kikristo, zingeondolewa mbali. Zingekoma. Lakini upendo utakuwepo sikuzote. Yehova ndiye chanzo cha upendo, naye anaishi milele. Hivyo, upendo hautashindwa kamwe, au kukoma. Utaendelea kuwepo milele ukiwa sifa ya Mungu wetu anayeishi milele.—1 Yoh. 4:8.

  • Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi Kamwe
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
    • Upendo Haushindwi Kamwe

      20, 21. (a) Kwa nini upendo ni wenye thamani bora zaidi? (b) Kwa nini umeazimia kufuatia ile njia ya upendo?

      20 Watu wa Yehova leo wanaonyesha kwamba ni jambo la hekima kufuatia ile njia iliyo bora zaidi ya upendo. Kwa kweli, njia hiyo inashinda hali yoyote ile. Ona jinsi mtume Paulo alivyokazia ukweli huo. Kwanza, alitaja kwamba zawadi za roho zingepitilia mbali na kwamba kutaniko la Kikristo lingekua na kufikia ukomavu. Kisha, akakata kauli hivi: “Sasa, hata hivyo, inabaki imani, tumaini, upendo, hayo matatu; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.”—1 Kor. 13:13.

      21 Mwishowe, mambo ambayo tunaamini yatakuwa halisi, na hivyo hatutahitaji tena kuonyesha imani katika mambo hayo. Tumaini katika ahadi ambazo tunatamani sana kuona zikitimizwa halitahitajiwa tena baada ya mambo yote kuwa mapya. Lakini namna gani upendo? Upendo hautashindwa kamwe, au kukoma. Utabaki.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki