Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usimamizi wa Kutimiza Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
    • “Siri Takatifu ya Mapenzi Yake”

      7. Yehova alifunua kusudi gani kupitia mtume Paulo?

      7 Katika barua aliyowaandikia Wakristo huko Efeso, mtume Paulo alieleza vizuri sana jinsi Yehova anavyosimamia mambo ili kutimiza kusudi lake. Paulo aliandika hivi: “Alitujulisha siri takatifu ya mapenzi yake. Ni kulingana na upendezi wake mwema alioukusudia ndani yake mwenyewe

  • Usimamizi wa Kutimiza Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
    • (Waefeso 1:9,

  • Usimamizi wa Kutimiza Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
    • 8. Ni nini maana ya neno linalotafsiriwa kuwa “usimamizi”?

      8 ‘Upendezi mwema’ wa Yehova, au kusudi lake, litatimizwa kupitia “usimamizi” fulani. Paulo alitumia neno ambalo, linapotafsiriwa moja kwa moja humaanisha “usimamizi wa nyumba.” Halirejelei serikali, kama vile Ufalme wa Kimasihi, bali linarejelea njia ya kusimamia mambo.b Njia bora ambayo Yehova angetumia kusimamia mambo ili kutimiza kusudi lake ilihusisha “siri takatifu” ambayo ingefunuliwa hatua kwa hatua kadiri wakati ulivyopita.—Waefeso 1:10; 3:9, maelezo ya chini katika Reference Bible.

      9. Yehova alifunuaje hatua kwa hatua siri takatifu ya mapenzi yake?

      9 Kupitia maagano mbalimbali yaliyofuatana, Yehova alifunua hatua kwa hatua jinsi ambavyo kusudi lake kuhusiana na Uzao ulioahidiwa huko Edeni lingetimizwa. Agano lake na Abrahamu lilifunua kwamba Uzao ulioahidiwa ungekuja duniani katika ukoo wa Abrahamu, na kupitia Uzao huo “mataifa yote ya dunia” yangejibariki. Agano hilo pia lilidokeza kwamba wengine wangeshirikiana na sehemu ya msingi ya uzao huo. (Mwanzo 22:17, 18) Agano la Sheria lililofanywa pamoja na taifa la Israeli la asili lilifunua kusudi la Yehova la kuwa na “ufalme wa makuhani.” (Kutoka 19:5, 6) Agano lililofanywa pamoja na Daudi lilionyesha kwamba Uzao huo ungekuwa Kichwa cha Ufalme mpaka wakati usio na kipimo. (2 Samweli 7:12, 13; Zaburi 89:3, 4) Baada ya agano la Sheria kuwaongoza Wayahudi kwa Masihi, Yehova alifunua mambo mengine kuhusu utimizo wa kusudi lake. (Wagalatia 3:19, 24) Wanadamu ambao wangeshirikiana na sehemu ya msingi ya uzao ndio wangefanyiza “ufalme wa makuhani” uliotabiriwa, nao wangeingizwa katika “agano jipya” wakiwa “Israeli” jipya, taifa la kiroho.—Yeremia 31:31-34; Waebrania 8:7-9.c

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki