Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jihadharini na Walimu Wasio wa Kweli!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 1
    • 1. Yuda alikuwa amenuia kuandika juu ya nini, na kwa nini alibadili habari yake?

      NI JAMBO la kushtua kama nini! Walimu wasio wa kweli katika kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza! (Mathayo 7:15; Matendo 20:29, 30) Yuda, ndugu nusu ya Yesu alijua hilo. Alisema kwamba alikuwa amenuia kuwaandikia waamini wenzake “juu ya wokovu ambao sisi twashika kwa shirika,” lakini akaeleza hivi: “Niliona ni lazima niwaandikie ili kuwahimiza kwa bidii mfanye pigano kali kwa ajili ya imani.” Kwa nini Yuda alibadili habari yake? Yeye alisema ni kwa sababu, “watu fulani wamepenyeza ndani [ya makutaniko] . . . wakigeuza fadhili isiyostahiliwa ya Mungu wetu kuwa sababu ya kujitetea kwa ajili ya mwenendo mlegevu.”—Yuda 3, 4.

      2. Kwa nini 2 Petro sura ya 2 na Yuda yafanana sana?

      2 Yaonekana, Yuda aliandika muda mfupi baada ya Petro kuandika barua yake ya pili. Bila shaka Yuda alijua sana juu ya barua hiyo. Kwa hakika, aliandika mawazo mengi yaliyofanana nayo katika barua yake mwenyewe ya kuhimiza yenye nguvu. Kwa hiyo, tuchunguzapo 2 Petro sura ya 2, tutaona jinsi ifananavyo na barua ya Yuda.

  • Jihadharini na Walimu Wasio wa Kweli!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 1
    • 8, 9. (a) Wakristo wa mapema waliathiriwa na kusababu gani kulikopotoka? (b) Kulingana na Yuda, baadhi ya watu makutanikoni walikuwa wakifanya nini?

      8 Msomi mmoja wa Biblia alionelea kwamba “Kanisani mlikuwemo wale waliopotosha fundisho la uzuri,” au ‘fadhili isiyostahiliwa.’ (Waefeso 1:5-7) Kulingana naye, wengine walijadili hivi: “Je, wasema kwamba [fadhili isiyostahiliwa] ya Mungu ni nyingi sana hivi kwamba yaweza kufunika kila dhambi? . . . Basi na tuendelee kutenda dhambi, kwa kuwa [fadhili isiyostahiliwa] ya Mungu yaweza kufutilia mbali kila dhambi. Kwa hakika kadiri tuzidivyo kutenda dhambi ndivyo [fadhili isiyostahiliwa] ya Mungu hupata fursa zaidi za kufanya kazi.” Je, umepata kusikia kusababu kulikopotoka kama huko?

      9 Mtume Paulo alipinga kufikiri kwenye kosa juu ya rehema ya Mungu alipouliza hivi: “Je, tutaendelea katika dhambi, ili fadhili isiyostahiliwa ipate kuzidi?” Pia aliuliza hivi: “Je, tutafanya dhambi kwa sababu hatuko chini ya sheria bali chini ya fadhili isiyostahiliwa?” Paulo ajibu kila moja ya maswali hayo kwa kukazia hivi: “Hilo lisitukie kamwe!” (Waroma 6:1, 2, 15) Kwa wazi, kama vile Yuda aoneleavyo, watu fulani-fulani walikuwa “wakigeuza fadhili isiyostahiliwa ya Mungu wetu kuwa sababu ya kujitetea kwa ajili ya mwenendo mlegevu.” Hata hivyo, Petro aandika kwamba kwa watu hao ‘uangamizo hausinzii.’—Yuda 4; 2 Petro 2:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki