Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Siku Hii Itakuwa Ukumbusho Kwenu”
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Desemba 15
    • 9. Kulingana na Kutoka 12:6, mwana-kondoo wa Pasaka alipaswa kuchinjwa wakati gani? (Tazama pia sanduku “Ni Wakati Gani wa Siku?”)

      9 Kulingana na kitabu kimoja (The Pentateuch and Haftorahs), andiko la Kutoka 12:6 linasema kwamba mwana-kondoo alipaswa kuchinjwa “katikati ya zile jioni mbili.” Tafsiri fulani za Biblia hutumia maneno hayohayo. Tafsiri nyingine, kama vile Tanakh ya Kiyahudi hutafsiri maneno hayo kuwa “saa za jioni.” Tafsiri nyingine husema “wakati wa jioni,” “giza linapoanza kuingia,” au “jua linapotua.” Kwa hiyo, mwana-kondoo alipaswa kuchinjwa baada ya jua kutua lakini kabla ya giza kuingia, mwanzo wa Nisani 14.

      10. Watu fulani husema mwana-kondoo alichinjwa wakati gani, lakini hilo linatokeza swali gani?

      10 Baadaye, Wayahudi fulani walifikiri kwamba ingechukua saa nyingi kuchinja wana-kondoo wote walioletwa hekaluni. Kwa hiyo, walielewa kwamba andiko la Kutoka 12:6 lilimaanisha mwisho wa Nisani 14, yaani, kuanzia jua linapoanza kushuka (baada ya saa sita mchana) hadi mwisho wa siku jua linapotua. Ikiwa ilimaanisha hivyo, basi mlo wa Pasaka ungeliwa wakati gani? Profesa Jonathan Klawans, mtaalamu wa dini ya kale ya Kiyahudi aliandika hivi: “Siku mpya huanza jua linapotua, hivyo dhabihu inatolewa siku ya 14 lakini mlo na sherehe ya Pasaka hufanywa siku ya 15, ingawa kitabu cha Kutoka hakitaji jambo hilo waziwazi.” Pia aliandika hivi: “Maandishi ya Marabi . . . hayasemi lolote kuhusu utaratibu uliofuatwa katika mlo wa Pasaka [Seder] kabla ya Hekalu kuharibiwa” mwaka wa 70 W.K.—Italiki ni zetu.

  • “Siku Hii Itakuwa Ukumbusho Kwenu”
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Desemba 15
    • Ni Wakati Gani Wa Siku?

      Mchambuzi Myahudi anayeitwa Marcus Kalisch (1828-1885) aliandika hivi: “Wazo hilo limekaziwa waziwazi na Ebn Ezra [rabi maarufu Mhispania, 1092-1167]: ‘Tuna jioni mbili; ya kwanza, jua linapotua . . . na ya pili, giza linapoingia; na katikati ya jioni hizo mbili kuna kipindi cha saa moja na dakika ishirini hivi;’ na maelezo hayo ambayo yanaonekana kuwa sahihi zaidi yanapatana pia na maoni ya Wakaraite na Wasamaria, na yamekubaliwa na watu wengi.” Wazo la kwamba mwana-kondoo alichinjwa mwanzoni mwa Nisani 14 linapatana na mwongozo ambao Waisraeli walipewa katika Kumbukumbu la Torati 16:6 kwamba dhabihu ya “pasaka” ilipaswa kutolewa ‘wakati wa jioni mara tu baada ya jua kutua, wakati uliowekwa wa kutoka Misri.’—Kut. 30:8; Hes. 9:3-5, 11.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki