Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Wewe Utajifunza Kutokana na Majira?
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Septemba 1
    • Jambo hilo lingeweza kuathiri maoni yako juu ya matukio ya Biblia. Ungeweza kusoma hivi juu ya jinsi Eliya alivyomweka rasmi mrithi wake: “Akamkuta Elisha mwana wa Shafati, aliyekuwa akilima [kwa plau, NW], mwenye jozi za ng’ombe kumi na mbili mbele yake.” (1 Wafalme 19:19) Wewe wafikiri hilo lilitukia katika mwezi gani, na nchi ingeonekanaje? Na kwenye Yohana 4:35, Yesu alisema: “Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? . . . Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.” Ingawa alitaja wakati fulani hususa, je! wewe waelewa ni lini?

  • Je! Wewe Utajifunza Kutokana na Majira?
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Septemba 1
    • Elisha alikuwa akishiriki katika shughuli kubwa ya kulima kwa plau alipoitwa awe nabii. Hiyo yaelekea kuweka wakati huo katika Tishri (Septemba-Oktoba), wakati ambapo joto kali mno la kiangazi lilikuwa limekwisha. Mvua za mapema zilikuwa zimeanza kulainisha udongo, zikiwezesha ulimaji wa plau, kufuatwa na upandaji.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki