-
Je! Wewe Utajifunza Kutokana na Majira?Mnara wa Mlinzi—1990 | Septemba 1
-
-
Jambo hilo lingeweza kuathiri maoni yako juu ya matukio ya Biblia. Ungeweza kusoma hivi juu ya jinsi Eliya alivyomweka rasmi mrithi wake: “Akamkuta Elisha mwana wa Shafati, aliyekuwa akilima [kwa plau, NW], mwenye jozi za ng’ombe kumi na mbili mbele yake.” (1 Wafalme 19:19) Wewe wafikiri hilo lilitukia katika mwezi gani, na nchi ingeonekanaje? Na kwenye Yohana 4:35, Yesu alisema: “Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? . . . Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.” Ingawa alitaja wakati fulani hususa, je! wewe waelewa ni lini?
-
-
Je! Wewe Utajifunza Kutokana na Majira?Mnara wa Mlinzi—1990 | Septemba 1
-
-
Elisha alikuwa akishiriki katika shughuli kubwa ya kulima kwa plau alipoitwa awe nabii. Hiyo yaelekea kuweka wakati huo katika Tishri (Septemba-Oktoba), wakati ambapo joto kali mno la kiangazi lilikuwa limekwisha. Mvua za mapema zilikuwa zimeanza kulainisha udongo, zikiwezesha ulimaji wa plau, kufuatwa na upandaji.
-