-
“Ni Nani Aliye Kama Yehova Mungu Wetu?”Mnara wa Mlinzi—1992 | Novemba 15
-
-
15. Huenda ikawa Zaburi 115 iliimbwaje?
15 Zaburi 115 hutuhimiza tumsifu na kumtumaini Yehova. Inamhesabia baraka na msaada na kuthibitisha kwamba sanamu hazifai kitu. Huenda ikawa kwamba zaburi hiyo iliimbwa kwa kuitikiana. Yaani, sauti moja huenda ikaimba: “Enyi mmchao BWANA [Yehova, NW], mtumainini BWANA [Yehova, NW].” Huenda ikawa kundi lilijibu: “Yeye ni msaada wao na ngao yao.”—Zaburi 115:11
-
-
“Ni Nani Aliye Kama Yehova Mungu Wetu?”Mnara wa Mlinzi—1992 | Novemba 15
-
-
17. Kwa kuwa wafu hawawezi kumsifu Yehova, sisi twapaswa kufanya nini, na kukiwa na matarajio gani?
17 Halafu himizo latolewa kumtumaini Yehova akiwa ndiye Msaidizi na Ngao ya ulinzi ya Israeli, ya nyumba ya Haruni ya kikuhani, na ya wote wanaomhofu Mungu. (Zaburi 115:9-11) Tukiwa wale wanaomhofu Yehova, tuna kicho kingi chenye staha kwa Mungu na hofu ifaayo ya kutompendeza. Pia tuna imani kwamba “Aliyezifanya mbingu na nchi” hubariki waabudu wake waaminifu-washikamanifu. (Mistari 12-15) Mbingu ndipo mahali pa kiti chake cha utawala, lakini Mungu aliifanya dunia iwe makao ya milele ya ainabinadamu yenye uaminifu-mshikamanifu na utii. Kwa kuwa wafu wanyamavu, wasio na ufahamu hawawezi kumsifu Yehova, sisi, tulio hai, twapaswa kufanya hivyo kwa ujitoaji na uaminifu-mshikamanifu kamili. (Mhubiri 9:5) Ni wale tu wanaomsifu Yehova watakaofurahia uhai wa milele na kuweza ‘kumbariki Yah’ milele, wakimsifu “hadi wakati usiojulikana.” Kwa hiyo acheni tujiunge kwa uaminifu-mshikamanifu pamoja na wale wanaotii lile himizo: “Sifuni Yah, enyi watu!”—Zaburi 115:16-18, NW.
-