Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tumaini Katika Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Desemba 15
    • 13, 14. Ni wapi ambapo Mashahidi wa Yehova wanaweka tumaini lao, na wao wanafanya nini juu yalo?

      13 Bila shaka. Yesu hajachukua mahali pa Yehova akiwa tumaini la aina ya wanadamu. Zaburi 37:34, NW bado inabaki ikitumika: “Tumaini katika Yehova na shika njia yake, naye atakweza wewe umiliki dunia. Wakati waovu wanapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.” Bado inahitajiwa kabisa kuendelea kutumaini katika Yehova na kutia moyo jamii zote za watu ziache kutumaini katika mashirika ya kibinadamu.

  • Tumaini Katika Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Desemba 15
    • 16. Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba Yesu alikuwa na mtazamo wa mambo unaofanana na ule ambao Daudi alikuwa nao?

      16 Mfalme Daudi alikuwa mchungaji wa kiroho wa Yehova kwa yale makabila ya Israeli wa kale, na yeye ndiye alitayarisha njia ili Yerusalemu uwe mji mkuu wa taifa hilo, ambapo Sulemani mwana wake alitawala kwa miaka 40. Kwa sababu nzuri, Yesu Kristo alinenwa kuwa ndiye ‘mwana wa Daudi.’ (Luka 1:31; 18:39; 20:41) Ikiwa Daudi alitumaini katika Yehova Mungu, Yesu Kristo mzao wake wa kidunia angefanya vivyo hivyo. Na alifanya.

      17. Kuna ithibati gani kwamba Yesu alitumaini katika Yehova?

      17 Kama ithibati ya kwamba mzao wa Daudi wa kidunia mwenye sifa zaidi ya wote, Yesu Kristo, alifuata shauri la Zaburi 37:34 wakati alipokuwa akipumua mpumuo wake wa mwisho juu ya mti wa mateso, Yesu alisema: “Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.” (Luka 23:46) Yeye alikuwa akitaja na kutimiza maneno ya Daudi kwenye Zaburi 31:5, ambayo yalielekezwa kwa Mungu: “Mikononi mwako naiweka roho yangu.” Tumaini la Yesu halikutamaushwa, kama vile la Mfalme Daudi halikutamaushwa. Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu siku ya tatu. Siku 40 baadaye yeye alirudi kwa Baba yake wa kimbingu. Kwenye mwisho wa Nyakati za Mataifa katika 1914, Yehova alikweza Mwana wake awe Mtawala wa dunia.

      Wakati wa Kuwa na Tumaini Sasa

      18. Kwa sababu gani leo ni wakati unaofaa wa kuwa na tumaini?

      18 Leo, wakati ule mwaka mpya 6,014 A.M. (katika ule Mwaka wa Ulimwengu) unaposogeza jamaa ya kibinadamu mbele kuingia wakati ujao, ni tumaini gani linaloweza kuwapo kwa ajili ya jamaa ya kibinadamu? Swali hilo linafaa sana sasa kwa sababu karibu miaka 1,900 sisi tumo ndani ya ile pindi ya baada ya Biblia kuandikwa. Umekuwa muda mrefu tangu Daudi aandike Zaburi 37:34.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki