Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Wewe Unafanya Mapenzi ya Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—1994 | Machi 1
    • Kudumisha Shangwe ya Kufanya Mapenzi ya Mungu

      Mfalme Daudi wa Israeli ya kale ni mmoja aliyejaribu kufanya mapenzi ya Mungu muda wote wa maisha yake. Yajapokuwa magumu na mibano mingi iliyoletwa dhidi yake, alipuliziwa kusema hivi: “Kufanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; naam, sheria yako imo moyoni mwangu.” (Zaburi 40:8) Kufanya mapenzi ya Yehova kulikuwa ndani kabisa ya nafsi ya Daudi, katika kiumbe chake mwenyewe. Hiyo ilikuwa ndiyo siri ya shangwe yake isiyofifia katika kumtumikia Yehova. Kufanya mapenzi ya Mungu hakukuwa jambo gumu kwa Daudi. Badala ya hivyo, lilikuwa jambo lenye kupendeza, jambo lililotoka moyoni mwake. Muda wote wa maisha yake, aling’ang’ana kufanya vizuri awezavyo kumtumikia Mungu wake, Yehova, hata ingawa nyakati nyingine alifanya dhambi na kupungukiwa.

      Pindi kwa pindi, huenda shangwe yetu ikapunguka. Huenda tukachoka au kushuka moyo. Labda yale yaliyotukia zamani yaendelea kutuletea matatizo, dhamiri yetu ikitusumbua juu ya tendo fulani baya lililofanywa zamani sana. Mara nyingi, twaweza kushinda hisia hizo kwa kujifunza Neno la Mungu kwa ukamili zaidi. Twaweza kuwa na lengo la kuandika sheria ya Mungu ‘moyoni mwetu,’ kama vile Daudi alivyofanya. Tukijaribu kufanya mapenzi ya Mungu kwa moyo wote, yaani, vizuri tuwezavyo, yeye atatuthawabisha kulingana na hayo kwa sababu yeye ni mwaminifu.—Waefeso 6:6; Waebrania 6:10-12; 1 Petro 4:19.

      Kwa kupendeza, kwenye Waebrania 10:5-7, mtume Paulo alinukuu maneno ya Daudi kwenye Zaburi 40:6-8 akayatumia kuhusu Yesu Kristo. Kwa kufanya hivyo, Paulo alionyesha jinsi Yesu alivyokuwa karibu na Babake. Neno la Kiebrania “mapenzi” huwa na mawazo ya ‘jambo la kupendeza, tamaa, upendeleo, au upendezi.’ Kwa hiyo, Zaburi 40:8 laweza kusomwa hivi kuhusu Kristo: “Nimependezwa, Ee Mungu wangu, kufanya upendezi wako.”a Yesu alitaka kufanya yale ambayo yalimpendeza Babake. Yesu alifanya zaidi ya yale aliyotakiwa afanye. Alifanya yale yaliyokuwa karibu na moyo wa Babake, na alionea shangwe kuyafanya.

      Maisha yote ya Yesu yalikazia kufundisha wengine mapenzi ya Mungu na yale waliyopaswa wafanye ili kupata baraka ya Mungu. Yeye alikuwa mhubiri na mwalimu wa wakati wote na alipata shangwe kuu katika kufanya kazi hiyo. Kwa hiyo yafuatana kwamba kadiri tufanyavyo kazi ya Yehova kwa wingi zaidi, ndivyo tutakavyopokea shangwe nyingi zaidi. Je! wewe pia waweza kutumikia wakati wote katika kazi ya kuhubiri ili shangwe yako iongezeke pia?

  • Je! Wewe Unafanya Mapenzi ya Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—1994 | Machi 1
    • a Ona kielezi-chini cha Zaburi 40:8, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki