-
“Hekima Ni Ulinzi”Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 15
-
-
Kuwa na hekima kuna uvutano gani juu ya usemi wetu? Mfalme mwenye hekima anatuambia hivi: “Anayetumia ufahamu katika jambo atapata mema, naye anayemtegemea Yehova ni mwenye furaha. Mtu mwenye hekima moyoni itasemwa kwamba ana uelewaji, naye mwenye midomo mitamu huongeza ushawishi. Ufahamu ni kisima cha uzima kwa hao walio nao; nayo nidhamu ya wapumbavu ni upumbavu. Moyo wa mtu mwenye hekima hukifanya kinywa chake kionyeshe ufahamu, na kwenye midomo yake huongeza ushawishi.”—Methali 16:20-23.
-
-
“Hekima Ni Ulinzi”Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 15
-
-
Haishangazi kwamba “mtu mwenye hekima moyoni” anaitwa “mwenye akili” au “mwenye utambuzi”! (Methali 16:21, An American Translation; New International Version) Ndiyo, ufahamu ni “kisima cha uzima” kwa wale walio nao. Lakini namna gani wapumbavu? ‘Wanadharau hekima na nidhamu.’ (Methali 1:7) Wanapata matokeo gani wanapokataa nidhamu ya Yehova? Kama ilivyoonyeshwa hapo juu, Sulemani anasema: “nidhamu ya wapumbavu ni upumbavu.” (Methali 16:22) Kwa kawaida wanapata nidhamu zaidi, wanapoadhibiwa vikali. Wapumbavu wanaweza pia kujiletea matatizo, aibu, magonjwa, na hata kifo cha mapema.
-