-
“Mwogope Mungu wa Kweli na Kushika Amri Zake”Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
-
-
Soma sura 9 na 10. Uhai ni wenye thamani kubwa, na Mungu anatutaka sisi tuufurahie (9:4, 7). Kwa kuwa sisi hatuna uongozi juu ya matokeo ya maisha (9:11, 12), ni vizuri zaidi kutii hekima ya kimungu, ingawa watu walio wengi hawaithamini (9:17). Kwa sababu ya mashaka-mashaka ya maisha, inatupasa tulinde moyo wetu (10:2) tujizoeze tahadhari katika yote tunayofanya, na kutenda kwa hekima yenye mafaa.—10:8-10.
-
-
“Mwogope Mungu wa Kweli na Kushika Amri Zake”Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
-
-
◆ 10:2, NW—Ni jinsi gani moyo uko kwenye mkono wa kuume?
“Mkono wa kuume” mara nyingi unaonyesha hali ya upendeleo. (Mathayo 25:33) Kwa hiyo uhakika wa kwamba moyo wa mtu mwenye hekima uko “kwenye mkono wa kuume wake” unaonyesha kwamba huo unamsukuma afuatie mwendo mwema, ulio na upendeleo. Lakini mpumbavu hana kusudio jema na anatenda kipumbavu na isivyofaa. Kuwa na moyo wake “mkono wa kushoto” wake kunaonyesha kwamba yeye anasukumwa kufuata kijia kibaya.
-