-
“Mwogope Mungu wa Kweli na Kushika Amri Zake”Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
-
-
Soma sura 9 na 10. Uhai ni wenye thamani kubwa, na Mungu anatutaka sisi tuufurahie (9:4, 7). Kwa kuwa sisi hatuna uongozi juu ya matokeo ya maisha (9:11, 12), ni vizuri zaidi kutii hekima ya kimungu, ingawa watu walio wengi hawaithamini (9:17). Kwa sababu ya mashaka-mashaka ya maisha, inatupasa tulinde moyo wetu (10:2) tujizoeze tahadhari katika yote tunayofanya, na kutenda kwa hekima yenye mafaa.—10:8-10.
-
-
“Mwogope Mungu wa Kweli na Kushika Amri Zake”Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
-
-
Somo kwetu sisi: Kwa kuwa kifo cha ghafula kinaweza kuangukia ye yote kati yetu (9:12), inatupasa tuwe tukitumia maisha yetu katika utumishi wa Yehova ikiwa kifo chetu kitatukia kisimamishe kila kitu (9:10). Tunahitaji pia kuwa wenye ujuzi mwingi katika utumishi wetu kwa sababu kutoweza kazi, hata katika mambo yale mepesi kama kuchimba shimo au kupasua miti, kunaweza kutudhuru sisi wenyewe na wengine.—10:8, 9.
-