-
“Mwogope Mungu wa Kweli na Kushika Amri Zake”Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
-
-
Jambo linalofanya kitabu hiki kivutie sana ni zile namna nyingi sana za habari ambazo mwandikaji anachimbua—hekima na utawala wa kibinadamu, utajiri wa vitu vya kimwili na anasa, dini ya kidesturi tu, na kadhalika. Mambo yote hayo ni ubatili, kwa maana si ya kudumu. Kwa upande ule mwingine, kuyatafakari kunaiongoza akili yenye kuona mambo ikate shauri moja tu: “Mwogope Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwa maana huo ndio wajibu mzima wa mwanadamu.”—Mhubiri 12:13, NW.
-
-
“Mwogope Mungu wa Kweli na Kushika Amri Zake”Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
-
-
Somo kwetu sisi: Kama Sulemani, inatupasa sisi tutafakari juu ya yale ambayo Neno la Mungu linasema juu ya maisha. Ndipo azimio letu la kuogopa na kutii Mungu litakapotiwa nguvu. Kujua kwamba Yehova anatuhangaikia kindani (12:13, 14) kunatuvuta karibu zaidi naye.
Basi, sisi na ‘tumwogope Mungu wa kweli na kushika amri zake.’ Huo ndio wajibu wetu na utatuletea furaha inayodumu.
-