-
“Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
13. Yehova anatoa unabii gani juu ya Mtumishi wake Mteule?
13 Isaya anaendelea kusema hivi: “Mungu BWANA anena, yeye aliyeziumba mbingu, na kuzitanda; yeye aliyeitandaza nchi na mazao yake; yeye awapaye pumzi watu walio juu yake; yeye awapaye roho wao waendao ndani yake.” (Isaya 42:5) Lo, hayo ni maelezo yenye mkazo kama nini juu ya Yehova, Muumba! Kikumbusha hicho juu ya uweza wa Yehova kinakazia maneno yake. Yehova anasema hivi: “Mimi, BWANA, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa; kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa.”—Isaya 42:6, 7.
-
-
“Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
15, 16. Yesu alitumikiaje akiwa “nuru ya mataifa”?
15 Akiwa “nuru ya mataifa,” Mtumishi aliyeahidiwa ‘atafunua macho ya vipofu’ na kuwakomboa “wale walioketi gizani.” Ndivyo Yesu alivyofanya. Yesu alitukuza jina la Baba yake wa kimbingu kwa kuishuhudia kweli. (Yohana 17:4, 6) Alifunua wazi uwongo mwingi wa kidini, akahubiri habari njema za Ufalme, akawafungulia mlango wa uhuru wa kiroho wale waliokuwa katika utumwa wa kidini. (Mathayo 15:3-9; Luka 4:43; Yohana 18:37) Alitoa onyo la kutofanya kazi za giza na kumfichua Shetani kuwa “baba ya uwongo” na “mtawala wa ulimwengu huu.”—Yohana 3:19-21; 8:44; 16:11.
16 Yesu alisema hivi: “Mimi ni nuru ya ulimwengu.” (Yohana 8:12) Alipata kuwa nuru hiyo kwa njia ya wazi sana alipotoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kuwa fidia. Hivyo aliwafungulia njia wale wenye kudhihirisha imani ili wapate msamaha wa dhambi, uhusiano unaokubalika pamoja na Mungu, na tazamio la uhai wa milele. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Kwa kuendeleza ujitoaji mkamilifu wa kimungu maisha yake yote, Yesu aliiunga mkono enzi kuu ya Yehova, akathibitisha Ibilisi ni mwongo. Kweli Yesu alikuwa mfunguaji wa macho ya vipofu, na mkombozi wa wale waliotiwa katika gereza la giza la kiroho.
-