-
Mungu Ni Nani?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
1. Mungu anaitwa nani, na ni nini kinachoonyesha kwamba anataka tulijue jina lake?
Mungu anajitambulisha kwetu kupitia Biblia. Anasema: “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu.” (Soma Isaya 42:5, 8.) Jina “Yehova” limetafsiriwa kutoka katika Kiebrania na linamaanisha “Yeye Husababisha Kuwa.” Yehova anataka ulijue jina lake, na ulitumie. (Kutoka 3:15) Tunajuaje jambo hilo? Alihakikisha kwamba jina lake linapatikana zaidi ya mara 7,000 katika Biblia!a Jina Yehova ni la “Mungu wa kweli juu mbinguni na chini duniani.”—Kumbukumbu la Torati 4:39.
-
-
Ni Ibada Gani Inayokubalika kwa Mungu?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Tunapaswa kumwabudu Yehova jinsi gani?
Tunapaswa kumwabudu Yehova peke yake kwa sababu yeye ndiye Muumba wetu. (Ufunuo 4:11) Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kumpenda na kumwabudu yeye peke yake, bila kutumia sanamu, mifano, au picha.—Soma Isaya 42:8.
Ibada yetu inapaswa kuwa “takatifu na yenye kukubalika” kwa Yehova. (Waroma 12:1) Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kuishi kulingana na viwango vyake vya maadili. Kwa mfano, wale wanaompenda Yehova wanapenda na kufuata viwango vyake kuhusu ndoa. Pia, wanaepuka mazoea yasiyofaa kama vile kuvuta sigara, kutumia dawa za kulevya au kunywa pombe kupita kiasi.a
-