Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mtumaini Yehova Ukabilipo Janga
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 26, 27. (a) Isaya atabiri matukio gani? (b) Maneno ya Isaya yaonyesha nini kwa watumishi wa Yehova leo?

      26 Isaya aendelea na maonyo yake: “Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Shiloa yapitayo polepole, na kufurahi kwa ajili ya Resini na huyo mwana wa Remalia, basi sasa angalia; Bwana aleta juu yao maji ya huo Mto, yenye nguvu, mengi sana, nayo ni mfalme wa Ashuru na utukufu wake wote; naye atakuja, na kupita juu ya mifereji yake yote, atafurika juu ya kingo zake zote; naye atapita, atapita kwa kasi na kuingia Yuda; atafurika na kupita katikati, atafika hata shingoni; na kule kuyanyosha mabawa yake kutaujaza upana wa nchi yako, Ee Imanueli.”—Isaya 8:5-8.

      27 “Watu hawa,” ufalme wa kaskazini wa Israeli, wakataa agano la Yehova na Daudi. (2 Wafalme 17:16-18) Kwa maoni yao, agano hilo ni hafifu kama maji yanayotiririka ya Shiloa, mfereji unaoleta maji Yerusalemu. Wanafurahia vita yao dhidi ya Yuda. Lakini dharau hilo halitakosa kuadhibiwa. Yehova atawaruhusu Waashuri ‘wafurike,’ au wapindue, Siria na Israeli, kama vile Yehova atakavyoiruhusu sehemu ya kisiasa ya ulimwengu ifurike milki ya dini isiyo ya kweli. (Ufunuo 17:16; linganisha Danieli 9:26.) Kisha, Isaya asema, “maji” yanayofurika “[y]atapita kwa kasi na kuingia Yuda,” na kufika “hata shingoni,” hadi Yerusalemu, ambako kichwa (mfalme) cha Yuda chatawala.b Katika wakati wetu, vivyo hivyo wafishaji wa kisiasa wa dini isiyo ya kweli watavamia watumishi wa Yehova na kuwazingira “hata shingoni.” (Ezekieli 38:2, 10-16) Tokeo litakuwa nini? Basi, ni nini kinachotukia wakati wa Isaya? Je, Waashuri wafurika kupitia kuta za jiji na kuwafagilia mbali watu wa Mungu? La. Mungu yuko pamoja nao.

  • Mtumaini Yehova Ukabilipo Janga
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • b Ashuru pia yafananishwa na ndege ambaye mabawa yake yaliyonyoshwa “[ya]ujaza upana wa nchi yako.” Kwa hiyo, jeshi la Ashuru litajaza pembe zote za nchi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki