-
Ufalme Unatimiza Mapenzi ya Mungu DunianiUfalme wa Mungu Unatawala!
-
-
9, 10. (a) Unabii ulio kwenye Isaya 11:6-9 unatimizwaje leo? (b) Tunaona uthibitisho gani kwamba kuna amani miongoni mwa watu wa Mungu?
9 Usalama. Katika unabii ulioandikwa kwenye Isaya 11:6-9, tunapata picha ya upatano na amani—kati ya wanyama-mwitu na wanadamu pamoja na wanyama wao wa kufugwa. Je, picha hiyo inatimizwa kwa njia ya kiroho leo? Ndiyo! Katika mstari wa 9, tunajifunza ni kwa nini wanyama hao hawatasababisha madhara wala uharibifu: “Kwa maana dunia hakika itajawa na kumjua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.” Je, “kumjua Yehova” kunabadili tabia za wanyama? Hapana. Watu ndio wanaobadilika wanapomjua Mungu Aliye Juu Zaidi na kujifunza kuiga njia zake zenye amani. Hiyo ndiyo sababu katika paradiso yetu ya kiroho leo, tunaweza kuona jinsi ambavyo unabii huo umetimizwa katika njia inayochangamsha moyo. Chini ya utawala wa Ufalme, wafuasi wa Kristo wanajifunza kuacha tabia zao za kikatili na za kinyama na kuishi kwa amani na upatano pamoja na ndugu na dada zao wa kiroho.
10 Kwa mfano, katika kitabu hiki, tumezungumza kuhusu msimamo wa Wakristo wa kutounga mkono upande wowote—tumezungumzia msingi wa Kimaandiko wa uelewaji wetu na jinsi ambavyo watu wa Mungu wameteswa kwa sababu ya kushikilia msimamo huo. Je, haishangazi kwamba katika ulimwengu huu wenye jeuri, kuna “taifa” la watu wengi kiasi ambao hukataa, hata wanapotishwa kuuawa, kujihusisha katika jeuri ya aina yoyote? Huo ni uthibitisho wa kutosha kuonyesha kwamba raia wa Ufalme wa Kimasihi kwa kweli wanafurahia amani kama ile iliyotajwa na Isaya! Yesu alisema kwamba wafuasi wake wangetambuliwa kwa upendo ambao wangekuwa nao miongoni mwao. (Yoh. 13:34, 35) Katika kutaniko, kwa subira, Kristo anamtumia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kuwafundisha Wakristo wote wa kweli kuwa wenye kufanya amani, upendo, na wapole.—Mt. 24:45-47.
-
-
Ufalme Unatimiza Mapenzi ya Mungu DunianiUfalme wa Mungu Unatawala!
-
-
16. Biblia inaelezaje usalama tutakaofurahia katika Paradiso?
16 Usalama. Hatimaye, maneno yenye kuchangamsha moyo yanayopatikana kwenye Isaya 11:6-9 yatatimia kwa ukamili katika njia halisi. Wanaume, wanawake, na watoto watakuwa salama salimini mahali popote duniani. Hakuna kiumbe yeyote, iwe mwanadamu au mnyama, atakayewatisha. Hebu wazia wakati ambapo dunia nzima itakuwa makao yako na utaweza kuogelea katika mito, maziwa, na bahari; kupanda milima; na kutembea mbugani bila woga wowote. Na wakati wa usiku, hutakuwa na wasiwasi wowote. Maneno ya Ezekieli 34:25 yatatimia, hivi kwamba watu wa Mungu wataweza ‘kukaa nyikani kwa usalama na kulala katika misitu.’
-