-
Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
-
-
24-26. Mashahidi wa Yehova wanashirikije katika utimizo wa unabii wa Isaya?
24 Mfalme Daudi aliandika kwamba wakati ambapo huyo Mesiya angeanza kutawala, ‘watu wa Mungu wangejitolea kwa moyo wa kupenda.’ (Zaburi 110:3, NW) Ijapokuwa hali za ulimwengu zimezidi kuwa mbaya tangu mwaka huo uliotiwa alama wa 1914, kumekuwako pia utimizo wa upande mzuri wa unabii huo; watu wa Mungu wamejitolea kwa moyo wa kupenda wakati wao ili kuhubiri hizi ‘habari njema za ufalme katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushahidi kwa mataifa yote.’ (Mathayo 24:14, NW) Kwa mfano, kila mwaka Mashahidi hutumia mamia ya mamilioni ya saa wakiongea na watu juu ya Ufalme wa Mungu na kuongoza mafunzo ya Biblia nyumbani bila malipo pamoja na wale wenye kupendezwa katika kuchunguza mambo ya hakika.
25 Wakati huo wote hutolewa bila malipo. Wale wenye kufanya kazi hiyo watoka katika kila namna ya maisha, wa umri wote, na kutoka karibu kila namna ya kazi iwazikayo. Hao ndio waelezwao kwenye Isaya 2:3 kwa maneno haya: “Na watu wa vikundi vingi watakwenda na kusema: ‘Njoni, acheni sisi tupande kwenye Mlima wa BWANA, [Kiebrania, יהזה, Yehova].’” Hiyo si kampeni tu ya “kupata nafsi.” Ni programu ya elimu ya ulimwenguni pote yenye malengo mawili: (1) Kuarifu watu wa kila taifa kwamba Ufalme wa Mungu unatawala na kuwaambia jambo hususa ambalo utafanya hivi karibuni, na (2) kuelimisha, bila malipo, wale wote wanaotaka kuchunguza mambo ya hakika na kumtumikia Mungu aliye hai kulingana na matakwa yake. Fanikio la kazi hii na utimizo wa unabii vimehakikishwa. Kwa nini? Kwa sababu Yehova Mungu mwenyewe anaiunga mkono.—Zekaria 4:6.
26 Je! si jambo la akili kuona kazi ya Mashahidi wa Yehova kuwa utimizo wa unabii kwenye Isaya 2:3? Je! wewe wajua mtu mwingine yeyote anayefanya kazi hii? Au wafikiri ni tukio la nasibu tu kwamba mamilioni ya watu hutafuta wakati katika maisha zao ili kuongea juu ya ujumbe uliotolewa unabii miaka elfu mbili hivi iliyopita, ujumbe ambao ungetangazwa katika pindi ya wakati wa msukosuko usio na kifani? Ndiyo, katika siku hizi za mwisho, Mashahidi wa Yehova ndio wamekuwa ‘nuru kwa mataifa.’ (Isaya 42:6; 49:6) Wao ndio udugu wa kimataifa pekee utumikiao Yehova Mungu kwa umoja na kwa amani chini ya mwelekezo wa Mesiya, lile “shina la Yese,” ambaye wanamtangaza kuwa ‘kionyo’ kwa mataifa.—Isaya 11:10, NW, JP.
Mashahidi wa Yehova, waonekanao hapa kando ya Bahari ya Galilaya, Israeli, wanatenda pia ulimwenguni pote, wakiwaalika watu wa mataifa yote wajifunze zaidi juu ya makusudi na matakwa ya Mungu
-
-
Ulimwengu Usio na Vita—Wewe Waweza KuuonaJe! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
-
-
3 Unabii uleule wa Yesu uliotoa ishara ya siku za mwisho ulikazia pia ukaribu wa kujiingiza kwa Mungu katika mambo ya wanadamu. Yesu alisema: “Kizazi hiki [kile kizazi cha 1914 ambacho kilishuhudia mwisho wa “zile nyakati zilizowekwa za mataifa”] hakitapita kamwe hata mambo haya yote yatukie.” (Mathayo 24:34; Luka 21:24, NW) Kizazi hicho chakaribia sana kupitilia mbali. Ndiyo, sasa ndio wakati wa uamuzi kwa ainabinadamu yote! Sasa, katika siku hizi za mwisho, au “mwisho wa siku,” (JP) ni lazima sisi tuchague kama ‘tutapanda kwenda kwenye mlima wa Yehova’ ‘tukafunzwe katika njia Zake’ au la. Lakini kama vile tumeona kutokana na mazungumzo haya, mengi zaidi yahusika katika kuja kumjua Mungu wa kweli, ‘katika kufunzwa katika njia Zake, katika kutembea katika vijia Vyake.’ (Isaya 2:2, 3, NW, Ta) Kufanya hivyo si jambo tu la kusoma broshua hii au kuchukua mtaala mfupi wa funzo. Yahusu kufunzwa kwenye kina kirefu zaidi kunakoathiri njia yote ya maisha ya mtu. Je! wewe ungependa kujua zaidi juu ya Mungu wa amani?
4 Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia ufanye uchunguzi mzito kama huo. Twakutia moyo uendelee kuchunguza habari hii kwa bidii yote ya moyo, ili wewe pia uweze kuwa miongoni mwa wale ‘wapandao kwenda kwenye mlima wa Yehova, wafunzwao katika vijia Vyake.’ Ili kupata msaada zaidi, onana na Mashahidi wa Yehova kwenye Jumba la Ufalme au ofisi ya tawi iliyo karibu nawe, Matokeo yenye kuridhisha yanaelezwa vizuri na nabii Mika: “Nao kwa kweli wataketi, kila mmoja chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, na hapatakuwa na yeyote wa kuwafanya wateteme.” Wewe na uwe miongoni mwa wale ambao ‘hutembea katika jina la Yehova milele’ katika ulimwengu usio na vita!—Mika 4:4, 5, NW.
-