Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Masomo Kutokana na Hekalu Aliloona Ezekieli
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • “Hii Ndiyo Sheria ya Hekalu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Maono ya Ezekieli Yanatufundisha Nini Leo?

      Wanyama waliotolewa dhabihu kwenye hekalu aliloona Ezekieli.

      SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 13A: Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti

      13, 14. (a) Tunajuaje kwamba maono ya hekalu aliloona Ezekieli yanatimizwa katika siku zetu? (b) Tunafaidika kwa njia gani mbili na maono hayo leo? (Tazama sanduku 13A, “Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti.”)

      13 Je, tunaweza kuwa na uhakika kwamba hekalu aliloona Ezekieli linatuhusu leo? Ndiyo! Kumbuka uhusiano kati ya maono ya Ezekieli kuhusu nyumba takatifu ya Mungu juu ya “mlima mrefu sana” na unabii wa Isaya kwamba “mlima wa nyumba ya Yehova” ungeimarishwa “kabisa juu ya vilele vya milima.” Isaya alisema kihususa kwamba unabii wake ungetimizwa “siku za mwisho,” au “katika kipindi cha mwisho cha zile siku.” (Eze. 40:2; Isa. 2:2-4; maelezo ya chini; tazama pia Mika 4:1-4.) Unabii huo unahusu kipindi cha siku za mwisho tangu 1919 ibada safi ilipoinuliwa, na kurudishwa, kana kwamba imewekwa juu ya mlima mrefu sana.b

      14 Basi ni wazi kabisa kwamba maono ya Ezekieli yanahusiana na ibada safi leo. Kama maono hayo yalivyowanufaisha wahamishwa Wayahudi nyakati za kale, yanatunufaisha leo kwa njia mbili. (1) Tunapata masomo muhimu kuhusu jinsi ya kufuata viwango vya Yehova katika ibada safi. (2) Tunapata uhakikisho wa kinabii kuhusu kurudishwa kwa ibada safi na baraka za Yehova.

  • Masomo Kutokana na Hekalu Aliloona Ezekieli
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Mchoro unaoonyesha sehemu kuu za hekalu la Ezekieli. Sehemu hizo zinatia ndani: 1. Mlima mrefu. 2. Ukuta. 3. Eneo pana kuzunguka majengo ya hekalu. 4. Mto unaotiririka kutoka patakatifu pa hekalu. 5. Malango ya nje. 6. Ukuta wa majengo ya hekalu. 7. Ua wa nje. 8. Vyumba vya nje vya kulia chakula. 9. Malango ya ndani. 10. Ua wa ndani 11. Madhabahu. 12. Patakatifu pa hekalu. Ndege kubwa zaidi ya kubeba abiria (ina urefu wa mita 75 hivi) inaonyeshwa kama ulinganisho wa ukubwa na ni ndogo sana kwa kulinganisha na ukuta unaozunguka eneo kubwa la hekalu (urefu wa mita 1,555 hivi).

      Ibada Safi Yainuliwa na Kulindwa

      Hekalu hilo limekwezwa juu ya “mlima mrefu sana” (1). Je, tumeiinua ibada safi, na kuitanguliza kabisa katika maisha yetu?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki