-
“Hii Ndiyo Sheria ya Hekalu”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
Maono ya Ezekieli Yanatufundisha Nini Leo?
13, 14. (a) Tunajuaje kwamba maono ya hekalu aliloona Ezekieli yanatimizwa katika siku zetu? (b) Tunafaidika kwa njia gani mbili na maono hayo leo? (Tazama sanduku 13A, “Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti.”)
13 Je, tunaweza kuwa na uhakika kwamba hekalu aliloona Ezekieli linatuhusu leo? Ndiyo! Kumbuka uhusiano kati ya maono ya Ezekieli kuhusu nyumba takatifu ya Mungu juu ya “mlima mrefu sana” na unabii wa Isaya kwamba “mlima wa nyumba ya Yehova” ungeimarishwa “kabisa juu ya vilele vya milima.” Isaya alisema kihususa kwamba unabii wake ungetimizwa “siku za mwisho,” au “katika kipindi cha mwisho cha zile siku.” (Eze. 40:2; Isa. 2:2-4; maelezo ya chini; tazama pia Mika 4:1-4.) Unabii huo unahusu kipindi cha siku za mwisho tangu 1919 ibada safi ilipoinuliwa, na kurudishwa, kana kwamba imewekwa juu ya mlima mrefu sana.b
14 Basi ni wazi kabisa kwamba maono ya Ezekieli yanahusiana na ibada safi leo. Kama maono hayo yalivyowanufaisha wahamishwa Wayahudi nyakati za kale, yanatunufaisha leo kwa njia mbili. (1) Tunapata masomo muhimu kuhusu jinsi ya kufuata viwango vya Yehova katika ibada safi. (2) Tunapata uhakikisho wa kinabii kuhusu kurudishwa kwa ibada safi na baraka za Yehova.
-
-
Masomo Kutokana na Hekalu Aliloona EzekieliHatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
Ibada Safi Yainuliwa na Kulindwa
Hekalu hilo limekwezwa juu ya “mlima mrefu sana” (1). Je, tumeiinua ibada safi, na kuitanguliza kabisa katika maisha yetu?
-