Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Kuwaleta Wengi Kwenye Uadilifu’
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Septemba
    • 6. Ni nini kitakachotokea baada ya umati mkubwa kuokoka dhiki kuu? Eleza. (Tazama pia katika toleo hili “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” kuhusu ufufuo kwenye uhai hapa duniani.)

      6 Soma Danieli 12:2. Ni nini kinachotokea baada ya umati mkubwa kuokoka kipindi cha taabu? Unabii huu hauzungumzii ufufuo wa mfano, yaani, kufanywa hai tena kiroho kwa watumishi wa Mungu kunakotokea katika siku za mwisho, kama tulivyoelewa zamani.c Badala yake, maneno haya yanarejelea ufufuo wa wafu utakaofanywa katika ulimwengu mpya unaokuja. Kwa nini tunasema hivyo? Neno “mavumbuni” linatumiwa pia kwenye Ayubu 17:16 kumaanisha “Kaburi.” Hilo linaonyesha kwamba Danieli 12:2 inazungumzia ufufuo halisi ambao utafanywa baada ya siku za mwisho kwisha na baada ya vita vya Har–Magedoni.

      7. (a) Baadhi ya watu watafufuliwa na kupata “uzima wa milele” katika maana gani? (b) Kwa nini huo ni “ufufuo ulio bora”?

      7 Hata hivyo, andiko la Danieli 12:2 linamaanisha nini linaposema kwamba baadhi ya watu watafufuliwa na kupata “uzima wa milele”? Linamaanisha kwamba wale watakaofufuliwa na kumjua, au kuendelea kumjua, na kumtii Yehova na Yesu wakati wa ile miaka 1,000, hatimaye watapata uzima wa milele. (Yoh. 17:3) Huo utakuwa “ufufuo ulio bora” kuliko ufufuo uliofanywa zamani ambapo baadhi ya wanadamu walifufuliwa. (Ebr. 11:35) Kwa nini? Kwa sababu wanadamu hao wasio wakamilifu walikufa tena.

      8. Ni kwa njia gani wengine wanafufuliwa na kupata “shutuma na chuki ya milele”?

      8 Lakini si wote ambao watafufuliwa watakubali kufundishwa na Yehova. Unabii wa Danieli unasema kwamba baadhi ya watu watafufuliwa na kupata “shutuma na chuki ya milele.” Kwa kuwa wataonyesha mtazamo wa uasi, majina yao hayataandikwa katika kitabu cha uzima na hawatapata uzima wa milele. Badala yake, watapata “chuki ya milele,” au uharibifu. Basi Danieli 12:2 inazungumza kuhusu matokeo ya mwisho kwa wote watakaofufuliwa ikitegemea mambo watakayofanya baada ya kufufuliwa.d (Ufu. 20:12) Baadhi yao watapata uzima wa milele; na wengine hawatapata.

  • ‘Kuwaleta Wengi Kwenye Uadilifu’
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Septemba
    • a Makala hii inatoa uelewaji mpya kuhusu kazi kubwa ya kutoa elimu inayofafanuliwa kwenye Danieli 12:2, 3. Tutachunguza wakati ambao jambo hilo litatokea na wale watakaohusika. Pia, tutaona jinsi kazi hiyo ya kutoa elimu itakavyowatayarisha wale walio duniani kwa ajili ya jaribu la mwisho, mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Kristo.

  • ‘Kuwaleta Wengi Kwenye Uadilifu’
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Septemba
    • c Ufafanuzi huu unarekebisha uelewaji unaopatikana kwenye kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! sura ya 17, na gazeti Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 1987, uku. 21-25.

      d Kinyume chake, maneno “waadilifu” na “wasio waadilifu” kwenye Matendo 24:15 na maneno “wale waliotenda mema” na “wale waliozoea kutenda maovu” kwenye Yohana 5:29, yanazungumzia matendo ambayo wale watakaofufuliwa walifanya kabla ya kufa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki