-
Shambulizi Kutoka Kaskazini!Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2020 | Aprili
-
-
14. Unabii wa Yoeli 2:28, 29 ulitimizwaje?
14 Sasa, Yoeli ana habari njema za kutangaza. Nchi itatoa mazao yake tena. (Yoe. 2:23-26) Kisha wakati fulani ujao, chakula kingi cha kiroho kingepatikana. “Nitaimimina roho yangu juu ya kila aina ya mwili,” asema Yehova, “na wana wenu na mabinti wenu watatoa unabii . . . Na hata juu ya watumwa wangu wa kiume na watumwa wa kike nitaimimina roho yangu.” (Yoe. 2:28, 29) Kumiminwa kwa roho hiyo takatifu ya Mungu hakukutendeka mara tu baada ya Waisraeli kurudishwa katika nchi yao kutoka Babiloni. Badala yake, kulitendeka karne nyingi baadaye, kwenye Pentekoste 33 W.K. Tunajuaje?
15. Kulingana na Matendo 2:16, 17, Petro alitumia maneno gani tofauti kidogo aliponukuu Yoeli 2:28, na jambo hilo linaonyesha nini?
15 Akiongozwa na roho takatifu, mtume Petro alihusianisha utimizo wa Yoeli 2:28, 29 na tukio lenye kustaajabisha lililotendeka siku ya Pentekoste. Saa tatu hivi asubuhi hiyo, roho takatifu ilimiminwa kimuujiza na kuwafanya wale walioipokea waanze kuzungumza “kuhusu mambo makuu ya Mungu.” (Mdo. 2:11) Chini ya mwongozo wa roho takatifu, Petro alitumia maneno tofauti kidogo alipokuwa akinukuu unabii wa Yoeli. Je, ulitambua tofauti ya maneno aliyotumia? (Soma Matendo 2:16, 17.) Badala ya kuanza na neno “kisha” kama Yoeli alivyofanya, Petro alitumia maneno: “Na katika siku za mwisho”—katika muktadha huu akirejelea siku za mwisho za mfumo wa Kiyahudi—ambapo Mungu angemimina roho yake “juu ya kila aina ya mwili.” Hilo linaonyesha kwamba muda mrefu ungepita kabla ya kutimizwa kwa unabii wa Yoeli.
16. Roho ya Mungu ilitimiza nini kuhusiana na kazi ya kuhubiri katika karne ya kwanza, na vipi kuhusu leo?
16 Baada ya tukio hilo lenye kustaajabisha la kumiminwa kwa roho ya Mungu katika karne ya kwanza, kazi ya kuhubiri ilianza kuenea kwa kiwango kikubwa sana. Kufikia wakati ambapo mtume Paulo aliandika barua yake kwa Wakolosai, karibu mwaka wa 61 W.K., angeweza kueleza kwamba habari njema ilikuwa imehubiriwa “katika uumbaji wote chini ya mbingu.” (Kol. 1:23) Katika siku za Paulo, maneno “uumbaji wote” yalimaanisha ulimwengu uliojulikana wakati huo. Kwa msaada wa roho takatifu ya Yehova yenye nguvu, kazi ya kuhubiri imefanywa kwa kiwango kikubwa hata zaidi katika siku zetu—“mpaka miisho ya dunia”!—Mdo. 13:47; tazama sanduku “Nitaimimina Roho Yangu.”
-