Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Acheni Wote Wamtukuze Yehova!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 1
    • 19. Twaweza kushirikije katika utimizo wa Hagai 2:6, 7?

      19 Pendeleo letu la kushiriki katika utimizo wa Hagai 2:6, 7 katika siku ya kisasa ni lenye shangwe: “BWANA wa majeshi asema hivi, Mara moja tena ni kitambo kidogo tu, nami nitazitikisa hizo mbingu, na hii nchi, na bahari, na nchi kavu; nami nitatikisa mataifa yote, na vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote vitakuja; nami nitaijaza nyumba hii utukufu, asema BWANA wa majeshi.” Pupa, ufisadi, na chuki zimeenea kotekote katika ulimwengu huu wa karne ya 20. Kwa kweli umo katika siku zao za mwisho, na Yehova ameanza tayari ‘kuutikisa’ kwa kuwaamuru Mashahidi wake ‘watangaze siku yake ya kisasi.’ (Isaya 61:2) Kutikisa huko kwa mwanzo kutafikia upeo kwa uharibifu wa ulimwengu kwenye Har–Magedoni, lakini kabla ya wakati huo, Yehova anakusanya “vitu vinavyotamaniwa na mataifa” kwa ajili ya utumishi wake—watu wa dunia walio wasikivu, wenye mfano wa kondoo. (Yohana 6:44) Sasa “umati mkubwa” huo ‘unatoa utumishi mtakatifu’ katika ua wa kidunia wa nyumba yake ya ibada.—Ufunuo 7:9, 15.

  • Utukufu Mkubwa Zaidi wa Nyumba ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 1
    • Utukufu Mkubwa Zaidi wa Nyumba ya Yehova

      “Nitaijaza nyumba hii utukufu, asema BWANA wa majeshi.”—HAGAI 2:7.

      1. Roho takatifu yahusianaje na imani na kazi?

      ALIPOKUWA akihubiri nyumba hadi nyumba, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikutana na bibi Mpentekoste aliyeeleza hivi, ‘Sisi tuna roho takatifu, lakini nyinyi ndio mnaofanya kazi.’ Kwa busara, alielezwa kwamba mtu aliye na roho takatifu hana budi kutiwa hamasa, kufanya kazi ya Mungu. Yakobo 2:17 lataarifu hivi: “Imani ikiwa haina kazi, imekufa ndani yayo yenyewe.” Kwa msaada wa roho ya Yehova, Mashahidi wake wamekuza imani yenye nguvu, naye ‘ameijaza nyumba yake utukufu’ kwa kuwaelekeza ili wafanye kazi zenye uadilifu—hasa ‘kuhubiri habari njema hii ya Ufalme katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya kuwa ushahidi kwa mataifa yote.’ Yehova aridhikapo na kufanywa kwa kazi hiyo, “ndipo mwisho utakapokuja.”—Mathayo 24:14.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki