-
Yehova Huchukia Mwenendo wa HilaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
16, 17. Watu fulani walifuata mwenendo gani wa hila?
16 Kisha Malaki ataja kosa la pili la hila: kumtendea vibaya mwenzi wa ndoa, hasa kwa kumtaliki bila sababu nzuri. Mstari wa 14 wa sura ya 2 wasema: “BWANA amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana [“hila,” NW], angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.” Kwa kuwatendea wake zao kwa hila, waume Wayahudi walifanya madhabahu ya Yehova ‘ifunikwe kwa machozi.’ (Malaki 2:13) Wanaume hao walikuwa wakiwataliki wake zao kwa sababu mbalimbali zisizo na msingi, wakiwaacha wake wa ujana wao isivyofaa, labda ili waoe wanawake wachanga zaidi au wanawake wapagani. Nao makuhani wafisadi waliruhusu jambo hilo! Hata hivyo, andiko la Malaki 2:16 linasema: “Nakuchukia kuachana, asema BWANA, Mungu wa Israeli.” Baadaye, Yesu alionyesha kwamba msingi pekee wa talaka ambao ungefanya mwenzi asiye na hatia awe huru kufunga ndoa, ni uasherati.—Mathayo 19:9.
-
-
Yehova Huchukia Mwenendo wa HilaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
18. Unabii wa Malaki kuhusu hila unatuhusuje leo?
18 Bila shaka, shauri hilo kuhusu masuala hayo linatuhusu leo. Ni jambo la kusikitisha kwamba watu fulani hupuuza mwongozo wa Mungu wa kufunga ndoa katika Bwana tu. Pia inasikitisha kwamba wengine hukosa kujitahidi kuimarisha ndoa yao. Badala yake, wao hutoa udhuru na kufuata mwenendo unaochukiwa na Mungu kwa kuwapa wenzi wao talaka zisizo za Kimaandiko ili kufunga ndoa na mtu mwingine. Kwa kufanya mambo hayo yote, wao ‘humchokesha Yehova.’ Katika siku za Malaki, wale waliopuuza mashauri ya Mungu hata walihisi kwa ushupavu kwamba maoni ya Yehova hayafai. Ni kama walisema: “Mungu mwenye kuhukumu yuko wapi?” Walikuwa na mawazo yaliyopotoka kama nini! Na tusinaswe na mtego huo.—Malaki 2:17.
-