-
Matayarisho ya Kukabiliana na MatesoMnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
-
-
“Zaidi,” Yesu aendelea, “ndugu atamtoa ndugu kwenye kifo, na baba mtoto wake, na watoto watainuka dhidi ya wazazi na watawafanya wauawe.” Anaongezea hivi: “Ninyi mtakuwa vitu vya kuchukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu; lakini yeye ambaye amevumilia mpaka mwisho ndiye ambaye ataokolewa.”
-
-
Matayarisho ya Kukabiliana na MatesoMnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
-
-
Ni kweli kwamba Yesu alitoa agizo hili, onyo, na kitia-moyo kwa mitume wake 12, lakini hayo pia yalikusudiwa kwa ajili ya wale ambao wangeshiriki katika kuhubiri ulimwenguni pote baada ya kifo na ufufuo wake. Hilo linaonyeshwa na uhakika wa kwamba yeye alisema wanafunzi wake ‘wangechukiwa na watu wote,’ si na Waisraeli pekee ambao kwao mitume walitumwa kuhubiri. Zaidi ya hilo, kwa wazi mitume hawakuitwa mbele ya magavana na wafalme wakati Yesu alipowatuma nje katika kampeni yao ya muda mfupi ya kuhubiri. Isitoshe, wakati huo waamini hawakutolewa kwenye kifo na washiriki wa jamaa zao.
-