-
“Akawasikitikia”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
3 Ingawa kuna makelele ya umati, Yesu anawasikia waombaji hao wakipaaza sauti. Atafanya nini? Ana mambo mengi akilini na moyoni. Juma la mwisho la maisha yake duniani linakaribia. Anajua atateswa na kuuawa kikatili Yerusalemu. Hata hivyo, hapuuzi vilio vyao vya kusihi. Anasimama na kuagiza kwamba waombaji hao waletwe kwake. Waombaji hao wanamsihi: “Bwana, tunataka macho yetu yafunguliwe.” Yesu ‘anawasikitikia,’ kisha anayagusa macho yao, nao wanaanza kuona tena.a Papo hapo, wanaanza kumfuata Yesu.—Luka 18:35-43; Mathayo 20:29-34.
-
-
“Akawasikitikia”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
a Inasemekana kwamba neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘sikitikia,’ ni mojawapo ya maneno ya Kigiriki yanayoonyesha kwa mkazo zaidi hisia ya huruma. Kitabu kimoja kinasema kwamba neno hilo linadokeza “si kusikitika tu unapomwona mtu akiteseka, bali pia kutaka sana kumtuliza na kumwondolea mateso yake.”
-