-
Somo Kuhusu Kuwa Macho—MabikiraYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu amekuwa akijibu maswali ya mitume wake kuhusu ishara ya kuwapo kwake na ya umalizio wa mfumo wa mambo. Akiwa na jambo hilo akilini, sasa anawapa himizo lenye hekima kwa kutumia mfano mwingine. Wale wanaoishi wakati wa kuwapo kwake wangeona utimizo wa mfano huo.
Anaanza kusimulia mfano huo hivi: “Ufalme wa mbinguni ni kama mabikira kumi waliochukua taa zao na kwenda kumpokea bwana harusi. Watano kati yao walikuwa wapumbavu, na watano walikuwa wenye busara.”—Mathayo 25:1, 2.
Yesu hamaanishi kwamba nusu ya wanafunzi wake wanaorithi Ufalme ni wapumbavu na nusu nyingine ni wenye busara. Badala yake, anamaanisha kwamba kuhusiana na Ufalme, kila mwanafunzi wake ana uwezo wa kuchagua kuwa macho au kukengeushwa. Hata hivyo, Yesu hana shaka kwamba kila mtumishi wake anaweza kuendelea kuwa mwaminifu na kupokea baraka kutoka kwa Baba yake.
Katika mfano huo, mabikira wote kumi wanaenda kumpokea bwana harusi na kujiunga na msafara wa harusi. Atakapowasili, mabikira watamwangazia njia kwa taa zao, wakimsifu anapomleta bibi harusi katika nyumba aliyotayarishiwa. Hata hivyo, hali inakuwaje?
-
-
Somo Kuhusu Kuwa Macho—MabikiraYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Mitume wanaweza kutambua kwamba bwana harusi ambaye Yesu anamtaja, ni Yesu mwenyewe. Hapo awali hata alijilinganisha na bwana harusi. (Luka 5:34, 35) Namna gani wale mabikira wenye busara? Alipokuwa akizungumza kuhusu “kundi dogo” ambao watapewa Ufalme, Yesu alitumia maneno haya: “Vaeni mavazi, muwe tayari na mwashe taa zenu.” (Luka 12:32, 35) Basi, katika mfano huu unaohusu mabikira, mitume wanaweza kuelewa kwamba Yesu anamaanisha wao wenyewe. Sasa Yesu anawasilisha ujumbe gani katika mfano huo?
-