-
“New World Translation” ya Utaalamu na Yenye Kufuatia HakiMnara wa Mlinzi—1991 | Machi 1
-
-
Kulingana na Mathayo 26:26 katika New World Translation, Yesu, wakati wa kuanzisha Chakula cha Jioni cha Bwana, asema hivi juu ya mkate ambao anapitishia wanafunzi wake: “Huu humaanisha mwili wangu.” Tafsiri nyingine nyingi hufasiri mstari huo hivi: “Huu ni mwili wangu,” na hilo linatumiwa kuunga mkono fundisho kwamba mwadhimisho wa Chakula cha Jioni cha Bwana unapoendelea, mkate unakuwa mnofu halisi wa Kristo. Neno linalotafsiriwa katika New World Translation kuwa “humaanisha” (es·tinʹ, namna ya ei·miʹ) linatoka kwenye neno la Kigiriki linalomaanisha “kuwa,” lakini linaweza pia kuwa na maana ya “kumaanisha.” Kwa hiyo, Greek-English Lexicon of the New Testament ya Thayer husema kwamba kitenzi hiki “mara nyingi ni s.n. [sawa na] kuonyesha, kumaanisha, -wa na maana.” Kwa kweli, “humaanisha” ni tafsiri yenye akili hapa. Yesu alipoanzisha Kijio cha Mwisho, mnofu wake ulikuwa bado kwenye mifupa yake, kwa hiyo mkate ungaliwezaje kuwa mnofu wake wa halisi?a
-
-
“New World Translation” ya Utaalamu na Yenye Kufuatia HakiMnara wa Mlinzi—1991 | Machi 1
-
-
a Katika Ufunuo 1:20, Mtafsiri Mjerumani Curt Stage alifasiri kitenzi icho hicho hivi: “Vinara saba vya taa humaanisha [ei·sinʹ] yale makundi saba.” Fritz Tillmann na Ludwig Thimme vile vile hulifasiri kuwa “humaanisha” [ei·sinʹ] katika Mathayo 12:7.
-