-
Endelea Kuutafuta Ufalme na Uadilifu wa MunguMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
1, 2. Waandishi na Mafarisayo waliyageuza kuwa nini matendo ambayo yenyewe yalikuwa mema, na Yesu aliwapa wafuasi wake onyo gani?
WAANDISHI na Mafarisayo walitafuta uadilifu kwa njia yao wenyewe, ambayo haikuwa njia ya Mungu. Isitoshe, walipofanya matendo ambayo yenyewe yalikuwa mema, waliyageuza yakawa matendo ya kiunafiki ili yaonwe na wanadamu. Walikuwa wakitumikia, si Mungu, bali majivuno yao wenyewe. Yesu alionya wanafunzi wake dhidi ya kisingizio hicho: “Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.”—Mathayo 6:1.
-
-
Endelea Kuutafuta Ufalme na Uadilifu wa MunguMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
3. (a) Waandishi na Mafarisayo walilipwaje kwa ukamili kwa sababu ya upaji wao? (b) Msimamo wa Yesu juu ya upaji ulikuwaje tofauti?
3 Neno la Kigiriki la kusema ‘wanapata kwa ukamili’ (a·peʹkho) lilikuwa neno lililoonekana mara nyingi katika risiti (stakabadhi) za kibiashara. Utumizi walo katika Mahubiri juu ya Mlima waonyesha kwamba “wamekwisha kupata thawabu yao,” yaani, “wametia sahihi risiti ya thawabu yao: haki yao ya kupokea thawabu yao imepatikana, sawasawa kabisa kana kwamba walikuwa tayari wametoa risiti ili waipate.” (An Expository Dictionary of New Testament Words, cha W. E. Vine) Zawadi kwa maskini ziliapizwa peupe katika barabara. Katika masinagogi majina ya wapaji yalitangazwa. Wale waliotoa kiasi kikubwa waliheshimiwa kwa njia maalumu kwa kupewa viti karibu na marabi wakati wa ibada. Walitoa ili waonwe na wanadamu; walionwa na kutukuzwa na wanadamu; kwa sababu hiyo, wangeweza kuipiga risiti hiyo muhuri wa kwamba “Imelipwa Kikamili” kwa sababu ya thawabu waliyopata kwa kutoa kwao. Msimamo wa Yesu ulikuwa tofauti kama nini! Toa “kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.”—Mathayo 6:3, 4; Mithali 19:17.
-