Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ishi Kupatana na Sala ya Mfano—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Juni 15
    • “BABA YETU ULIYE MBINGUNI”

      4. Maneno “Baba yetu” yanatukumbusha nini? Ni katika maana gani Wakristo wenye tumaini la kuishi duniani wanamwona Yehova kuwa “Baba”?

      4 Maneno “Baba yetu,” na si “Baba yangu,” yanatukumbusha kwamba sisi ni sehemu ya “ushirika mzima wa akina ndugu” ambao wanapendana kikweli. (1 Pet. 2:17) Hiyo ni baraka iliyoje! Yehova amewachagua Wakristo watiwa-mafuta wakaishi mbinguni na amewafanya kuwa wana Wake, hivyo wanamwona Yehova kuwa “Baba” yao katika maana kamili. (Rom. 8:15-17) Wakristo wenye tumaini la kuishi duniani wanaweza pia kumwona Yehova kuwa “Baba” yao. Yeye ndiye huwapa uhai na kutosheleza mahitaji ya waabudu wake wa kweli. Wale wenye tumaini la kuishi duniani watakuwa watoto wa Mungu kikamili watakapofikia ukamilifu na kuendelea kuwa waaminifu baada ya jaribu la mwisho.—Rom. 8:21; Ufu. 20:7, 8.

  • Ishi Kupatana na Sala ya Mfano—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Juni 15
    • “JINA LAKO NA LITAKASWE”

      7. Watu wa Mungu wamepewa heshima gani, lakini tunapaswa kufanya nini?

      7 Ni heshima kubwa sana kwetu kulijua jina la Mungu na kuitwa “watu kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 15:14; Isa. 43:10) Tunasali hivi kwa Baba yetu wa mbinguni: “Jina lako na litakaswe.” Kufanya hivyo kutatuchochea tumwombe Yehova atusaidie kuepuka maneno au matendo yanayoweza kulivunjia heshima jina lake takatifu. Hatupaswi kuwa kama watu fulani katika karne ya kwanza ambao walitenda kinyume cha mambo waliyohubiri. Mtume Paulo aliandika hivi kuwahusu: “Jina la Mungu linafanyiwa makufuru katikati ya mataifa kwa sababu yenu.”—Rom. 2:21-24.

      8, 9. Toa mfano unaoonyesha jinsi ambavyo Yehova huwabariki wale wanaotaka kulitakasa jina lake.

      8 Tunataka kulitakasa jina la Mungu. Dada mmoja nchini Norway ambaye mume wake alikufa mvulana wao alipokuwa na umri wa miaka miwili, anaeleza hivi: “Ulikuwa wakati mgumu sana maishani mwangu. Nilisali kila siku, karibu kila saa, nikimwomba Yehova anisaidie kuwa mtulivu ili nisifanye uamuzi wowote usiofaa au kuvunja uaminifu wangu, na hivyo kumpa Shetani sababu ya kumdhihaki Yehova. Nilitaka kulitakasa jina la Yehova, na nilitaka mwanangu amwone tena baba yake katika Paradiso.”—Met. 27:11.

      9 Je, Yehova alijibu sala za dada huyo? Bila shaka! Waamini wenzake walimtia moyo kwa kuwa alishirikiana nao kwa ukawaida. Miaka mitano baadaye aliolewa na mzee wa kutaniko. Leo mtoto wake ambaye ana umri wa miaka 20, ni ndugu aliyebatizwa. Anasema hivi: “Nina furaha sana, kwa kuwa mume wangu alinisaidia kumlea.”

      10. Yehova atafanya nini ili kulitakasa jina lake?

      10 Ni nini kinahitaji kufanywa ili jina la Mungu litakaswe na kuondolewa shutuma kabisa? Ni lazima Yehova awaondoe wale wote wanaopinga kimakusudi enzi yake kuu. (Soma Ezekieli 38:22, 23.) Halafu, hatua kwa hatua wanadamu watafanywa kuwa wakamilifu. Tunatazamia kwa hamu wakati huo ambapo viumbe wote wenye akili watalitakasa jina la Yehova! Hatimaye, Baba yetu wa mbinguni atakuwa “vitu vyote kwa kila mtu.”—1 Kor. 15:28.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki