-
Amerudi Nyumbani Katika KapernaumuMnara wa Mlinzi—1986 | Mei 1
-
-
Yesu anapokuwa akifundisha mkutano wa watu, watu wanne wanaleta nyumbani mle mwanamume aliyepooza akiwa katika machela. Wanataka Yesu amponye rafiki yao, lakini kwa sababu ya mkutano wa watu wanashindwa kuingia ndani. Inakatisha tamaa kama nini! Hata hivyo wao hawazimii moyo. Wanapanda juu darini, wanatoboa shimo kwa kuviondoa vigae, na kuiteremsha machela iliyo na yule mwanamume aliyepooza na kuifikisha pale pale alipo Yesu.
Je, Yesu anakasirika kwa sababu ya kukatizwa hivyo? Hata kidogo! Bali, yeye anavutwa sana na imani yao. Anamwambia yule aliyepooza: “Umesamehewa dhambi zako.” Lakini je, Yesu kweli anaweza kusamehe dhambi? Waandishi na Mafarisayo hawafikiri hivyo. Wanawaza mioyoni mwao: “Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu? ”
-
-
Amerudi Nyumbani Katika KapernaumuMnara wa Mlinzi—1986 | Mei 1
-
-
[Picha ya ukurasa nzima katika ukurasa wa 8]
-