-
“Akawasikitikia”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
15, 16. Eleza visa viwili vinavyoonyesha maoni ya Yesu kuhusu watu ambao aliwahubiria.
15 Mwaka wa 31 W.K., baada ya kujikakamua katika huduma kwa miaka miwili hivi, Yesu aliongeza jitihada zake kwa “kutembelea majiji na vijiji vyote” huko Galilaya. Mambo aliyoyaona yalimgusa moyo. Mtume Mathayo anasimulia hivi: “Alipouona umati akawasikitikia, kwa sababu walikuwa wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.” (Mathayo 9:35, 36) Yesu aliwahurumia watu wa kawaida. Alijua vizuri kwamba wako katika hali mbaya ya kiroho. Alifahamu kwamba walikuwa wakitendewa vibaya na kupuuzwa kabisa na viongozi wa dini ambao walipaswa kuwa wachungaji wao. Akichochewa na huruma nyingi, Yesu alijitahidi sana kuwapa watu hao ujumbe wa tumaini. Walichohitaji hasa ni habari njema ya Ufalme wa Mungu.
-
-
“Akawasikitikia”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
18 Tunahitaji kuwaona watu kama Yesu alivyowaona, kwamba “wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.” Hebu wazia umempata mwana-kondoo aliyepotea. Kwa kuwa hana mchungaji wa kumwongoza malishoni na kwenye maji, kiumbe huyo mwenye kusikitisha ana njaa na kiu. Je, hungemhurumia sana mwana-kondoo huyo? Je, hungejitahidi juu chini kumpa chakula na maji? Mwana-kondoo huyo ni kama watu wengi ambao bado hawaijui habari njema. Kwa kuwa wamepuuzwa na wachungaji bandia wa dini, wana njaa na kiu ya kiroho, nao hawana tumaini la kweli la wakati ujao. Tuna kile wanachohitaji, yaani, chakula cha kiroho chenye afya na maji ya kweli yenye kuburudisha yaliyo katika Neno la Mungu. (Isaya 55:1, 2) Tunapofikiria mahitaji ya kiroho ya watu walio karibu nasi, tunawahurumia sana. Tukiwahurumia watu sana kama alivyofanya Yesu, tutajitahidi juu chini kuwaeleza tumaini la Ufalme.
-