-
Yehova ‘Atasababisha Haki Ifanywe’Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
8 Baada ya kutoa mfano huo, Yesu alieleza maana yake: “Sikieni lile ambalo mwamuzi huyo, ijapokuwa si mwadilifu, alisema! Basi, kwa hakika je, Mungu hatasababisha haki ifanywe kwa ajili ya watu wake waliochaguliwa ambao wanampaazia sauti mchana na usiku, hata ingawa ana ustahimilivu kwao? Ninawaambia ninyi, Yeye atasababisha watendewe haki upesi. Hata hivyo, Mwana wa binadamu atakapofika, je, kwa kweli ataipata imani duniani?”—Luka 18:1-8.
-
-
Yehova ‘Atasababisha Haki Ifanywe’Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
9. Ni jambo gani kuu linalokaziwa katika mfano wa mjane na mwamuzi?
9 Jambo kuu katika mfano huo liko wazi kabisa. Linatajwa na wale wanaohusika katika mfano huo na Yesu pia. Mjane alisihi hivi: “Hakikisha kwamba nitapata haki.” Mwamuzi huyo akasema: “Nitahakikisha kwamba atapata haki.” Yesu akauliza: “Je, Mungu hatasababisha haki ifanywe?” Na kumhusu Yehova, Yesu alisema hivi: “Yeye atasababisha watendewe haki upesi.” (Luka 18:3, 5, 7, 8) Ni wakati gani hasa Mungu ‘atasababisha haki ifanywe’?
10. (a) Haki ilifanywa wakati gani katika karne ya kwanza? (b) Haki itafanywa kwa ajili ya watu wa Mungu wakati gani na jinsi gani?
10 Katika karne ya kwanza, “siku za kupatiliza haki” (au “siku za kisasi,” Kingdom Interlinear) zilifika mwaka wa 70 W.K., Yerusalemu na hekalu lake lilipoharibiwa. (Luka 21:22) Kwa watu wa Mungu leo, haki itafanywa katika “ile siku kuu ya Yehova.” (Sefania 1:14; Mathayo 24:21) Wakati huo, Yehova ‘atawalipa dhiki wale wanaowafanyia dhiki’ watu wake, “[Yesu Kristo] anapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.”—2 Wathesalonike 1:6-8; Waroma 12:19.
-
-
Yehova ‘Atasababisha Haki Ifanywe’Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
12, 13. (a) Mfano wa Yesu wa mjane na mwamuzi unatufundisha somo jinsi gani? (b) Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atasikiliza sala zetu na kusababisha haki ifanywe?
12 Mfano wa Yesu wa mjane na mwamuzi unakazia kweli nyingine muhimu. Yesu alieleza maana ya mfano huo kwa kusema hivi: “Sikieni lile ambalo mwamuzi huyo, ijapokuwa si mwadilifu, alisema! Basi, kwa hakika je, Mungu hatasababisha haki ifanywe kwa ajili ya watu wake waliochaguliwa?” Bila shaka, Yesu hakuwa akimlinganisha Yehova na mwamuzi huyo kana kwamba Mungu angewatendea hivyo wale wanaomwamini. Badala yake, Yesu aliwafundisha wafuasi wake jambo fulani kumhusu Yehova kwa kukazia tofauti kati ya mwamuzi huyo na Mungu. Yehova na mwamuzi huyo wanatofautiana katika njia gani?
13 Mwamuzi katika mfano wa Yesu “si mwadilifu,” lakini “Mungu ni Mwamuzi mwadilifu.” (Zaburi 7:11; 33:5) Mwamuzi huyo hakumjali mjane huyo kibinafsi, lakini Yehova anamjali kila mtu mmoja-mmoja. (2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30) Mwamuzi hakuwa na nia ya kumsaidia yule mjane, lakini Yehova ana nia, ndiyo, anataka sana kuwasaidia wale ambao wanamtumikia. (Isaya 30:18, 19) Tunajifunza nini? Ikiwa mwamuzi asiye mwadilifu alisikiliza maombi ya mjane na kumfanyia haki, je, Yehova hatasikiliza hata zaidi sala za watu wake na bila shaka kusababisha haki ifanywe kwa ajili yao?—Methali 15:29.
14. Kwa nini hatupaswi kuacha kuamini kuja kwa siku ya Mungu ya hukumu?
14 Kwa hiyo, wale wanaoacha kuamini kuja kwa siku ya Mungu ya hukumu wanafanya kosa zito sana. Kwa nini? Kwa kuacha imani yao thabiti ya kwamba “siku kuu ya Yehova” imekaribia, wanatilia shaka uwezo wa Yehova wa kutimiza ahadi zake kwa uaminifu. Lakini hakuna mtu aliye na haki ya kutilia shaka uaminifu wa Mungu. (Ayubu 9:12) Swali linalofaa ni, Je, sisi binafsi tutaendelea kuwa waaminifu? Na hilo hasa ndilo jambo ambalo Yesu alikazia mwishoni mwa mfano wake wa mjane na mwamuzi.
-