Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kusaidia Mtoto Akue Katika Hekima ya Kutii Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Februari 15
    • Kusaidia Mtoto Akue Katika Hekima ya Kutii Mungu

      WATU wenye kufikiri wa mataifa na malezi mengi wanakubali kwamba Yesu alikuwa mwalimu na mfuata-adili aliye mzuri ajabu. Lakini je! mambo fulani katika mazoezi yake ujanani yalichangia jambo hilo? Ni masomo gani ambayo wazazi leo wanaweza kujifunza kutokana na maisha na malezi yake ya kijamaa?

      Biblia inatuambia machache sana juu ya utoto wa Yesu. Kwa msingi, miaka yake 12 ya kwanza inazungumzwa na kumalizwa kwa mistari miwili: “Kwa hiyo wakati [Yusufu na Mariamu] walipokuwa wametekeleza mambo yote kulingana na sheria ya Yehova, wao walirudi katika Galilaya kwenye mji wao wenyewe Nazareti. Na mtoto yule mchanga akaendelea kukua na kupata nguvu, akiwa anajazwa hekima, na upendeleo wa Mungu ukaendelea kuwa juu yake.” (Luka 2:39, 40, NW) Lakini hapa pana masomo ya wazazi kujifunza.

      Mtoto huyo mchanga ‘aliendelea kukua na kupata nguvu.’ Kwa sababu hiyo, wazazi wake walikuwa wakimtunza kimwili. Pia, yeye alikuwa ‘akijazwa hekima’ kwa kuendelea.a Lilikuwa daraka la nani kufundisha maarifa na ufahamu ambao ungekuwa msingi wa kupata hekima hiyo?

      Chini ya Sheria ya Musa, wazazi wake ndio waliokuwa na wajibu huo. Sheria hiyo iliambia wazazi Waisraeli hivi: “Na maneno haya ambayo mimi ninakuamuru wewe leo lazima yathibitike kuwa juu ya moyo wako; na wewe lazima uyakaze-kaze kikiki katika mwana wako na kusema juu yayo wakati wewe unaketi katika nyumba yako na wakati wewe unatembea katika barabara na wakati wewe unalala na wakati wewe unaamka.” (Kumbukumbu 6:6, 7, NW) Uhakika wa kwamba Yesu aliendelea ‘kujazwa hekima,’ na pia kwamba ‘upendeleo wa Mungu uliendelea kuwa juu yake,’ unaonyesha kwamba Yusufu na Mariamu walikuwa wakitii amri hiyo.

      Huenda wengine wakahisi kwamba kwa kuwa Yesu alikuwa mtoto mkamilifu, kwa kweli malezi yake hayaandai kiolezo kinachofaa kufuatwa kwa malezi ya watoto wengine. Ijapokuwa hivyo, Yusufu na Mariamu hawakuwa wakamilifu. Hata hivyo, kwa wazi wao waliendelea kumtolea mahitaji yake ya kimwili na kiroho, na walifanya hivyo wajapopatwa na mikazo ya jamaa yenye kukua. (Mathayo 13:55, 56) Pia, ingawa Yesu alikuwa mkamilifu, bado alipaswa akue kutoka utoto mchanga kupitia utoto mkubwa na kubalehe mpaka mtu mzima. Wazazi wake walikuwa na kazi nyingi ya kumfinyanga, na kwa wazi waliifanya vizuri.

  • Kusaidia Mtoto Akue Katika Hekima ya Kutii Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Februari 15
    • a Neno la kiasili la Kigiriki lina wazo la kwamba “kujawa na hekima” kwa Yesu kulikuwa kwa njia ya sikuzote, yenye kuendelea.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki