Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Tunda la Roho’ Linamtukuza Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Aprili 15
    • 3. (a) Tunamtukuza Mungu jinsi gani tunapositawisha ‘tunda la roho’? (b) Tutachunguza maswali gani?

      3 Sifa ambazo roho takatifu inatokeza zinaonyesha utu halisi wa Chanzo cha roho hiyo, yaani, Yehova Mungu. (Kol. 3:9, 10) Yesu alionyesha sababu ya msingi inayopaswa kuwafanya Wakristo wajitahidi kumwiga Mungu alipowaambia mitume wake hivi: “Baba yangu hutukuzwa katika hili, kwamba mwendelee kuzaa matunda mengi.”a (Yoh. 15:8) Tunapositawisha ‘tunda la roho,’ matokeo yanaonekana wazi kupitia jinsi tunavyosema na kutenda; na hilo linamletea Mungu wetu sifa. (Mt. 5:16) Tunda la roho linatofautiana katika njia gani na tabia za ulimwengu wa Shetani? Tunaweza kusitawisha jinsi gani tunda la roho? Kwa nini inaweza kuwa vigumu kwetu kufanya hivyo? Tutachunguza maswali au maulizo hayo tunapozungumzia sifa tatu za kwanza za tunda la roho, yaani, upendo, shangwe, na amani.

  • ‘Tunda la Roho’ Linamtukuza Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Aprili 15
    • a Tunda ambalo Yesu alitaja linatia ndani ‘tunda la roho’ na “tunda la midomo” ambalo Wakristo wanamtolea Mungu kupitia kazi ya kuhubiri Ufalme.—Ebr. 13:15.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki