-
‘Utunze Mzabibu Huu’!Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
-
-
Kama vile Yehova alivyowafananisha Waisraeli na mzabibu, Yesu alitumia mfano huohuo pia. Jioni ya mwisho ambayo Yesu alikuwa na wanafunzi wake, aliwaambia hivi: “Mimi ndiye mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.” (Yohana 15:1) Yesu aliwafananisha wanafunzi wake na matawi ya mzabibu. Kama vile matawi ya mzabibu halisi yanavyopata nguvu kutoka kwenye shina, wanafunzi wa Kristo wanapaswa kubaki katika muungano na yeye. Yesu alisema: “Bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe.” (Yohana 15:5) Wakulima hupanda mzabibu kwa sababu ya matunda yake, na Yehova anatazamia watu wake wazae matunda ya kiroho. Hilo humletea Mungu aliye Mkulima wa mzabibu uradhi na utukufu.—Yohana 15:8.
-
-
‘Utunze Mzabibu Huu’!Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
-
-
‘Endeleeni Kuzaa Matunda Mengi’
Matawi ya mfano ya “mzabibu wa kweli” yanawakilisha Wakristo watiwa-mafuta. Lakini, ni lazima “kondoo wengine” pia wathibitishe kwamba wao ni wafuasi wa Kristo wanaozaa matunda. (Yohana 10:16) Wao pia wanaweza kuzaa “matunda mengi” na kumpa utukufu Baba yao wa mbinguni. (Yohana 15:5, 8) Mfano wa Yesu wa mzabibu wa kweli hutukumbusha kwamba wokovu unategemea kubaki katika muungano pamoja na Kristo na kuzaa matunda mazuri ya kiroho. Yesu alisema: “Mkishika amri zangu, mtakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.”—Yohana 15:10.
-