Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Utunze Mzabibu Huu’!
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
    • Kama vile Yehova alivyowafananisha Waisraeli na mzabibu, Yesu alitumia mfano huohuo pia. Jioni ya mwisho ambayo Yesu alikuwa na wanafunzi wake, aliwaambia hivi: “Mimi ndiye mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.” (Yohana 15:1) Yesu aliwafananisha wanafunzi wake na matawi ya mzabibu. Kama vile matawi ya mzabibu halisi yanavyopata nguvu kutoka kwenye shina, wanafunzi wa Kristo wanapaswa kubaki katika muungano na yeye. Yesu alisema: “Bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe.” (Yohana 15:5) Wakulima hupanda mzabibu kwa sababu ya matunda yake, na Yehova anatazamia watu wake wazae matunda ya kiroho. Hilo humletea Mungu aliye Mkulima wa mzabibu uradhi na utukufu.—Yohana 15:8.

  • ‘Utunze Mzabibu Huu’!
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
    • ‘Endeleeni Kuzaa Matunda Mengi’

      Matawi ya mfano ya “mzabibu wa kweli” yanawakilisha Wakristo watiwa-mafuta. Lakini, ni lazima “kondoo wengine” pia wathibitishe kwamba wao ni wafuasi wa Kristo wanaozaa matunda. (Yohana 10:16) Wao pia wanaweza kuzaa “matunda mengi” na kumpa utukufu Baba yao wa mbinguni. (Yohana 15:5, 8) Mfano wa Yesu wa mzabibu wa kweli hutukumbusha kwamba wokovu unategemea kubaki katika muungano pamoja na Kristo na kuzaa matunda mazuri ya kiroho. Yesu alisema: “Mkishika amri zangu, mtakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.”—Yohana 15:10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki