-
‘Hakuna Mtu Mwingine Ambaye Amewahi Kuzungumza Hivyo’Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Baada ya kusikiliza mafundisho ya Yesu, baadhi yao wanasema: “Kwa kweli huyu ndiye Nabii,” inaelekea wanarejelea nabii aliyetabiriwa ambaye angekuwa mkuu kuliko Musa. Wengine wanasema: “Huyu ndiye Kristo.” Lakini wengine wanapinga na kusema: “Kristo hatakuja kutoka Galilaya, sivyo? Je, andiko halisemi kwamba Kristo atatoka katika uzao wa Daudi na atatoka Bethlehemu, kijiji alichoishi Daudi?”—Yohana 7:40-42.
-
-
‘Hakuna Mtu Mwingine Ambaye Amewahi Kuzungumza Hivyo’Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Maandiko hayasemi moja kwa moja kwamba nabii angetokea Galilaya. Hata hivyo Neno la Mungu lilionyesha kwamba Kristo angetokea huko; lilitabiri kwamba “nuru kuu” ingeonekana katika “Galilaya ya mataifa.” (Isaya 9:1, 2; Mathayo 4:13-17) Isitoshe, kama ilivyotabiriwa, Yesu alizaliwa huko Bethlehemu, naye ni mzao wa Daudi. Ingawa huenda Mafarisayo wanajua mambo hayo, inawezekana kwamba wao ndio wanaoeneza habari za uwongo kumhusu Yesu.
-