-
“Hakuna Hata Mmoja Wenu Atakayepotea”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
“Fadhili Zinazopita za Kawaida” (Mdo. 28:1-10)
18-20. Watu wa Malta walionyesha jinsi gani “fadhili zinazopita za kawaida,” na Mungu alifanya muujiza gani kupitia Paulo?
18 Waokokaji hao walijikuta katika kisiwa cha Malta, upande wa kusini wa Sisili. (Ona sanduku lenye kichwa “Kisiwa cha Malta Kilikuwa Wapi?”) Watu wa kisiwa hicho wanaozungumza lugha ya kigeni walionyesha “fadhili zinazopita za kawaida.” (Mdo. 28:2) Waliwasha moto kwa ajili ya watu hao wasiowajua waliofika pwani wakiwa wamelowa na kutetemeka kwa sababu ya baridi. Moto huo uliwasaidia kujipasha joto. Hali hiyo pia ilitokeza muujiza.
-