Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mungu Hana Ubaguzi”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 22, 23. Ndugu wa Antiokia walionyeshaje upendo wa kindugu, na watu wa Mungu leo wanaigaje mfano wao?

      22 Antiokia ndipo ambapo kwa mara ya kwanza “wanafunzi waliitwa Wakristo kupitia mwongozo wa Mungu.” (Mdo. 11:26b) Jina hilo lililotolewa kwa mwongozo wa Mungu liliwafaa watu hao waliofuata mfano wa Kristo katika maisha yao. Kadiri Watu wa Mataifa walivyokuwa wakijiunga na kutaniko la Kikristo, je, kulikuwa na umoja wa kindugu kati yao na Wayahudi? Fikiria kilichotokea wakati wa njaa kali ya karibu mwaka wa 46 W.K.e Wakati huo, njaa iliwaathiri hasa maskini ambao hawakuwa na akiba ya fedha wala chakula. Wakati huo wa njaa, Wakristo Wayahudi walioishi Yudea, ambao wengi wao walikuwa maskini, walihitaji msaada. Walipojua kwamba kuna uhitaji huo, akina ndugu huko Antiokia—kutia ndani Watu wa Mataifa waliokuwa Wakristo, ‘walituma msaada’ kwa akina ndugu walioishi Yudea. (Mdo. 11:29) Huo ulikuwa upendo wa kindugu!

  • “Mungu Hana Ubaguzi”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • e Mwanahistoria Myahudi Yosefo, aliandika kuhusu “njaa kali” iliyotokea wakati wa utawala wa Maliki Klaudio (41-54 W.K.).

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki