-
UadilifuUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Yosefu wa Arimathea alijulikana kuwa mtu “mwema na mwadilifu,” maneno hayo, bila shaka, hutumiwa kwa kawaida katika maana isiyo kamili kuwahusu wanadamu ambao hawajakamilika. (Lu 23:50; linganisha na Mt 19:16, 17; Mk 10:17, 18; tazama WEMA [Wema wa Yehova].) Amri za sheria ya Mungu kwa Waisraeli zilikuwa ‘takatifu [zilitoka kwa Mungu] na zenye uadilifu [zilifuata haki kamilifu] na njema [ziliwanufaisha katika kila sehemu ya maisha wale waliozifuata].”—Ro 7:12; linganisha na Efe 5:9.
-
-
UadilifuUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Sheria ilikuwa ya uadilifu. Hilo halimaanishi kwamba Sheria iliyotolewa kupitia Musa haikuwa na kiwango cha Mungu cha uadilifu. Ilikuwa nacho. Mtume Paulo anasema hivi: “Basi Sheria yenyewe ni takatifu, na amri ni takatifu na yenye uadilifu na ni njema.” (Ro 7:12; Kum 4:8) Ilitimiza kusudi la Mungu kwa kufanya makosa yawe wazi na kuwaongoza kwa Kristo Wayahudi waliokuwa na mioyo minyoofu, na vilevile ilikuwa na kivuli cha mambo mema ambayo yangekuja. (Gal 3:19, 24; Ebr 10:1) Lakini haingewawezesha wale walioifuata kuwa na uadilifu wa kweli ulio kamili. Wote walikuwa watenda dhambi; hawangeweza kutii Sheria hiyo kikamili; na kuhani mkuu wao hangeweza kuondoa dhambi zao kupitia dhabihu na utumishi wake. Kwa hiyo, wangeweza kuwa waadilifu kwa kukubali tu uandalizi wa Mungu wa kumtoa Mwana wake. (Ro 8:3, 4; Ebr 7:18-28) Wale waliomkubali Kristo walitangazwa kuwa waadilifu, si kama malipo kwao, bali kama zawadi, kisha Kristo akawa kwao “hekima kutoka kwa Mungu, pia uadilifu na utakaso na kuachiliwa huru kupitia fidia.” Hivyo, uadilifu wa kweli unaweza kupatikana tu kupitia Kristo. Jambo hilo linamkweza Yehova, nalo linamsifu yeye, wala si mwanadamu au kazi zake, kuwa Chanzo cha uadilifu wote, “ili iwe kama ilivyoandikwa: ‘Yule anayejisifu, na ajisifu katika Yehova.’”—1Ko 1:30, 31; Ro 5:17.
-